« Prev

76. Surah Al-Insân or Ad-Dahr سورة الإنسان

Next »




Ayah  76:1  الأية
    +/- -/+  
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
هَلْ أَتَىٰ عَلَى الْإِنسَانِ حِينٌ مِّنَ الدَّهْرِ لَمْ يَكُن شَيْئًا مَّذْكُورًا
Swahili
 
Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.

Ayah  76:2  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن نُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ نَّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَاهُ سَمِيعًا بَصِيرًا
Swahili
 
Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.

Ayah  76:3  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا هَدَيْنَاهُ السَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرًا وَإِمَّا كَفُورًا
Swahili
 
Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.

Ayah  76:4  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا أَعْتَدْنَا لِلْكَافِرِينَ سَلَاسِلَ وَأَغْلَالًا وَسَعِيرًا
Swahili
 
Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.

Ayah  76:5  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ الْأَبْرَارَ يَشْرَبُونَ مِن كَأْسٍ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا
Swahili
 
Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,

Ayah  76:6  الأية
    +/- -/+  
عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا عِبَادُ اللهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفْجِيرًا
Swahili
 
Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.

Ayah  76:7  الأية
    +/- -/+  
يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا
Swahili
 
Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,

Ayah  76:8  الأية
    +/- -/+  
وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا
Swahili
 
Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.

Ayah  76:9  الأية
    +/- -/+  
إِنَّمَا نُطْعِمُكُمْ لِوَجْهِ اللهِ لَا نُرِيدُ مِنكُمْ جَزَاءً وَلَا شُكُورًا
Swahili
 
Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.

Ayah  76:10  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا نَخَافُ مِن رَّبِّنَا يَوْمًا عَبُوسًا قَمْطَرِيرًا
Swahili
 
Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.

Ayah  76:11  الأية
    +/- -/+  
فَوَقَاهُمُ اللهُ شَرَّ ذَٰلِكَ الْيَوْمِ وَلَقَّاهُمْ نَضْرَةً وَسُرُورًا
Swahili
 
Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha na raha na furaha.

Ayah  76:12  الأية
    +/- -/+  
وَجَزَاهُم بِمَا صَبَرُوا جَنَّةً وَحَرِيرًا
Swahili
 
Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.

Ayah  76:13  الأية
    +/- -/+  
مُّتَّكِئِينَ فِيهَا عَلَى الْأَرَائِكِ ۖ لَا يَرَوْنَ فِيهَا شَمْسًا وَلَا زَمْهَرِيرًا
Swahili
 
Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.

Ayah  76:14  الأية
    +/- -/+  
وَدَانِيَةً عَلَيْهِمْ ظِلَالُهَا وَذُلِّلَتْ قُطُوفُهَا تَذْلِيلًا
Swahili
 
Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.

Ayah  76:15  الأية
    +/- -/+  
وَيُطَافُ عَلَيْهِم بِآنِيَةٍ مِّن فِضَّةٍ وَأَكْوَابٍ كَانَتْ قَوَارِيرَا
Swahili
 
Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,

Ayah  76:16  الأية
    +/- -/+  
قَوَارِيرَ مِن فِضَّةٍ قَدَّرُوهَا تَقْدِيرًا
Swahili
 
Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.

Ayah  76:17  الأية
    +/- -/+  
وَيُسْقَوْنَ فِيهَا كَأْسًا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا
Swahili
 
Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.

Ayah  76:18  الأية
    +/- -/+  
عَيْنًا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلْسَبِيلًا
Swahili
 
Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.

Ayah  76:19  الأية
    +/- -/+  
وَيَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيْتَهُمْ حَسِبْتَهُمْ لُؤْلُؤًا مَّنثُورًا
Swahili
 
Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.

Ayah  76:20  الأية
    +/- -/+  
وَإِذَا رَأَيْتَ ثَمَّ رَأَيْتَ نَعِيمًا وَمُلْكًا كَبِيرًا
Swahili
 
Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.

Ayah  76:21  الأية
    +/- -/+  
عَالِيَهُمْ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضْرٌ وَإِسْتَبْرَقٌ ۖ وَحُلُّوا أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٍ وَسَقَاهُمْ رَبُّهُمْ شَرَابًا طَهُورًا
Swahili
 
Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.

Ayah  76:22  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ هَٰذَا كَانَ لَكُمْ جَزَاءً وَكَانَ سَعْيُكُم مَّشْكُورًا
Swahili
 
Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.

Ayah  76:23  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا عَلَيْكَ الْقُرْآنَ تَنزِيلًا
Swahili
 
Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.

Ayah  76:24  الأية
    +/- -/+  
فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تُطِعْ مِنْهُمْ آثِمًا أَوْ كَفُورًا
Swahili
 
Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.

Ayah  76:25  الأية
    +/- -/+  
وَاذْكُرِ اسْمَ رَبِّكَ بُكْرَةً وَأَصِيلًا
Swahili
 
Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;

Ayah  76:26  الأية
    +/- -/+  
وَمِنَ اللَّيْلِ فَاسْجُدْ لَهُ وَسَبِّحْهُ لَيْلًا طَوِيلًا
Swahili
 
Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.

Ayah  76:27  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ هَٰؤُلَاءِ يُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ وَيَذَرُونَ وَرَاءَهُمْ يَوْمًا ثَقِيلًا
Swahili
 
Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.

Ayah  76:28  الأية
    +/- -/+  
نَّحْنُ خَلَقْنَاهُمْ وَشَدَدْنَا أَسْرَهُمْ ۖ وَإِذَا شِئْنَا بَدَّلْنَا أَمْثَالَهُمْ تَبْدِيلًا
Swahili
 
Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.

Ayah  76:29  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ هَٰذِهِ تَذْكِرَةٌ ۖ فَمَن شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ سَبِيلًا
Swahili
 
Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.

Ayah  76:30  الأية
    +/- -/+  
وَمَا تَشَاءُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللهُ ۚ إِنَّ اللهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمًا
Swahili
 
Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.

Ayah  76:31  الأية
    +/- -/+  
يُدْخِلُ مَن يَشَاءُ فِي رَحْمَتِهِ ۚ وَالظَّالِمِينَ أَعَدَّ لَهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا
Swahili
 
Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu.





© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us