1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
وَالذَّارِيَاتِ ذَرْوًا
Waththariyati tharwa
Swahili
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
|
Ayah 51:2 الأية
فَالْحَامِلَاتِ وِقْرًا
Falhamilati wiqra
Swahili
Na zinazo beba mizigo,
|
Ayah 51:3 الأية
فَالْجَارِيَاتِ يُسْرًا
Faljariyati yusra
Swahili
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
|
Ayah 51:4 الأية
فَالْمُقَسِّمَاتِ أَمْرًا
Falmuqassimati amra
Swahili
Na zinazo gawanya kwa amri,
|
Ayah 51:5 الأية
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ
Innama tooAAadoona lasadiq
Swahili
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
|
Ayah 51:6 الأية
وَإِنَّ الدِّينَ لَوَاقِعٌ
Wa-inna addeena lawaqiAA
Swahili
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
|
Ayah 51:7 الأية
وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْحُبُكِ
Wassama-i thati alhubuk
Swahili
Naapa kwa mbingu zenye njia,
|
Ayah 51:8 الأية
إِنَّكُمْ لَفِي قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ
Innakum lafee qawlin mukhtalif
Swahili
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
|
Ayah 51:9 الأية
يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ
Yu/faku AAanhu man ofik
Swahili
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
|
Ayah 51:10 الأية
قُتِلَ الْخَرَّاصُونَ
Qutila alkharrasoon
Swahili
Wazushi wameangamizwa.
|
Ayah 51:11 الأية
الَّذِينَ هُمْ فِي غَمْرَةٍ سَاهُونَ
Allatheena hum fee ghamratin sahoon
Swahili
Ambao wameghafilika katika ujinga.
|
Ayah 51:12 الأية
يَسْأَلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ الدِّينِ
Yas-aloona ayyana yawmu addeen
Swahili
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
|
Ayah 51:13 الأية
يَوْمَ هُمْ عَلَى النَّارِ يُفْتَنُونَ
Yawma hum AAala annariyuftanoon
Swahili
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
|
Ayah 51:14 الأية
ذُوقُوا فِتْنَتَكُمْ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تَسْتَعْجِلُونَ
Thooqoo fitnatakum hatha allatheekuntum bihi tastaAAjiloon
Swahili
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
|
Ayah 51:15 الأية
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Inna almuttaqeena fee jannatinwaAAuyoon
Swahili
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
|
Ayah 51:16 الأية
آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ
Akhitheena ma atahumrabbuhum innahum kanoo qabla thalika muhsineen
Swahili
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya
wakifanya mema.
|
Ayah 51:17 الأية
كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ
Kanoo qaleelan mina allayli mayahjaAAoon
Swahili
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
|
Ayah 51:18 الأية
وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ
Wabil-ashari humyastaghfiroon
Swahili
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
|
Ayah 51:19 الأية
وَفِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ
Wafee amwalihim haqqun lissa-iliwalmahroom
Swahili
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
|
Ayah 51:20 الأية
وَفِي الْأَرْضِ آيَاتٌ لِّلْمُوقِنِينَ
Wafee al-ardi ayatunlilmooqineen
Swahili
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
|
Ayah 51:21 الأية
وَفِي أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ
Wafee anfusikum afala tubsiroon
Swahili
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
|
Ayah 51:22 الأية
وَفِي السَّمَاءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ
Wafee assama-i rizqukum wamatooAAadoon
Swahili
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
|
Ayah 51:23 الأية
فَوَرَبِّ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِنَّهُ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَا أَنَّكُمْ
تَنطِقُونَ
Fawarabbi assama-i wal-ardiinnahu lahaqqun mithla ma annakum tantiqoon
Swahili
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo
kweli kuwa nyinyi mnasema.
|
Ayah 51:24 الأية
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ الْمُكْرَمِينَ
Hal ataka hadeethu dayfiibraheema almukrameen
Swahili
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
|
Ayah 51:25 الأية
إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلَامًا ۖ قَالَ سَلَامٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
Ith dakhaloo AAalayhi faqaloosalaman qala salamun qawmun munkaroon
Swahili
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu
nisio kujueni.
|
Ayah 51:26 الأية
فَرَاغَ إِلَىٰ أَهْلِهِ فَجَاءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ
Faragha ila ahlihi fajaabiAAijlin sameen
Swahili
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
|
Ayah 51:27 الأية
فَقَرَّبَهُ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Faqarrabahu ilayhim qala alata/kuloon
Swahili
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
|
Ayah 51:28 الأية
فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَامٍ
عَلِيمٍ
Faawjasa minhum kheefatan qaloo latakhaf wabashsharoohu bighulamin AAaleem
Swahili
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria
kupata kijana mwenye ilimu.
|
Ayah 51:29 الأية
فَأَقْبَلَتِ امْرَأَتُهُ فِي صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ
عَقِيمٌ
Faaqbalati imraatuhu fee sarratin fasakkatwajhaha waqalat AAajoozun AAaqeem
Swahili
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na
kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
|
Ayah 51:30 الأية
قَالُوا كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ
Qaloo kathaliki qalarabbuki innahu huwa alhakeemu alAAaleem
Swahili
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye
hikima na Mwenye kujua.
|
Ayah 51:31 الأية
قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ
Qala fama khatbukumayyuha almursaloon
Swahili
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
|
Ayah 51:32 الأية
قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
Qaloo inna orsilna ilaqawmin mujrimeen
Swahili
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
|
Ayah 51:33 الأية
لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ
Linursila AAalayhim hijaratanmin teen
Swahili
Tuwatupie mawe ya udongo,
|
Ayah 51:34 الأية
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ
Musawwamatan AAinda rabbika lilmusrifeen
Swahili
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
|
Ayah 51:35 الأية
فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Faakhrajna man kana feehamina almu/mineen
Swahili
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
|
Ayah 51:36 الأية
فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ الْمُسْلِمِينَ
Fama wajadna feehaghayra baytin mina almuslimeen
Swahili
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
|
Ayah 51:37 الأية
وَتَرَكْنَا فِيهَا آيَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ الْعَذَابَ الْأَلِيمَ
Watarakna feeha ayatanlillatheena yakhafoona alAAathaba al-aleem
Swahili
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
|
Ayah 51:38 الأية
وَفِي مُوسَىٰ إِذْ أَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ
Wafee moosa ith arsanahuila firAAawna bisultanin mubeen
Swahili
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
|
Ayah 51:39 الأية
فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِ وَقَالَ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
Fatawalla biruknihi waqala sahirunaw majnoon
Swahili
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au
mwendawazimu!
|
Ayah 51:40 الأية
فَأَخَذْنَاهُ وَجُنُودَهُ فَنَبَذْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ
Faakhathnahu wajunoodahufanabathnahum fee alyammi wahuwa muleem
Swahili
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa
kulaumiwa.
|
Ayah 51:41 الأية
وَفِي عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ الرِّيحَ الْعَقِيمَ
Wafee AAadin ith arsalnaAAalayhimu arreeha alAAaqeem
Swahili
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
|
Ayah 51:42 الأية
مَا تَذَرُ مِن شَيْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَالرَّمِيمِ
Ma tatharu min shay-in atatAAalayhi illa jaAAalat-hu karrameem
Swahili
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
|
Ayah 51:43 الأية
وَفِي ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا حَتَّىٰ حِينٍ
Wafee thamooda ith qeela lahumtamattaAAoo hatta heen
Swahili
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
|
Ayah 51:44 الأية
فَعَتَوْا عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ الصَّاعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ
FaAAataw AAan amri rabbihim faakhathat-humuassaAAiqatu wahum yanthuroon
Swahili
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
|
Ayah 51:45 الأية
فَمَا اسْتَطَاعُوا مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا مُنتَصِرِينَ
Fama istataAAoo min qiyaminwama kanoo muntasireen
Swahili
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
|
Ayah 51:46 الأية
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا فَاسِقِينَ
Waqawma noohin min qablu innahum kanooqawman fasiqeen
Swahili
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
|
Ayah 51:47 الأية
وَالسَّمَاءَ بَنَيْنَاهَا بِأَيْدٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ
Wassamaa banaynahabi-aydin wa-inna lamoosiAAoon
Swahili
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio
twenye uwezo wa kuzitanua.
|
Ayah 51:48 الأية
وَالْأَرْضَ فَرَشْنَاهَا فَنِعْمَ الْمَاهِدُونَ
Wal-arda farashnahafaniAAma almahidoon
Swahili
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
|
Ayah 51:49 الأية
وَمِن كُلِّ شَيْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
Wamin kulli shay-in khalaqna zawjaynilaAAallakum tathakkaroon
Swahili
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
|
Ayah 51:50 الأية
فَفِرُّوا إِلَى اللهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Fafirroo ila Allahi inneelakum minhu natheerun mubeen
Swahili
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha
nitokae kwake.
|
Ayah 51:51 الأية
وَلَا تَجْعَلُوا مَعَ اللهِ إِلَٰهًا آخَرَ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ
مُّبِينٌ
Wala tajAAaloo maAAa Allahi ilahanakhara innee lakum minhu natheerun mubeen
Swahili
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni
mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
|
Ayah 51:52 الأية
كَذَٰلِكَ مَا أَتَى الَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا سَاحِرٌ
أَوْ مَجْنُونٌ
Kathalika ma ata allatheenamin qablihim min rasoolin illa qaloo sahirunaw
majnoon
Swahili
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au
mwendawazimu.
|
Ayah 51:53 الأية
أَتَوَاصَوْا بِهِ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ
Atawasaw bihi bal hum qawmun taghoon
Swahili
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
|
Ayah 51:54 الأية
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَا أَنتَ بِمَلُومٍ
Fatawalla AAanhum fama anta bimaloom
Swahili
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
|
Ayah 51:55 الأية
وَذَكِّرْ فَإِنَّ الذِّكْرَىٰ تَنفَعُ الْمُؤْمِنِينَ
Wathakkir fa-inna aththikratanfaAAu almu/mineen
Swahili
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
|
Ayah 51:56 الأية
وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ
Wama khalaqtu aljinna wal-insailla liyaAAbudoon
Swahili
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
|
Ayah 51:57 الأية
مَا أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَا أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ
Ma oreedu minhum min rizqin wamaoreedu an yutAAimoon
Swahili
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
|
Ayah 51:58 الأية
إِنَّ اللهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ
Inna Allaha huwa arrazzaquthoo alquwwati almateen
Swahili
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
|
Ayah 51:59 الأية
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَابِهِمْ فَلَا
يَسْتَعْجِلُونِ
Fa-inna lillatheena thalamoothanooban mithla thanoobi as-habihimfala
yastaAAjiloon
Swahili
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi
wasinihimize.
|
Ayah 51:60 الأية
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِن يَوْمِهِمُ الَّذِي يُوعَدُونَ
Fawaylun lillatheena kafaroo minyawmihimu allathee yooAAadoon
Swahili
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|