Prev  

75. Surah Al-Qiyâmah سورة القيامة

  Next  



1st Ayah  1  الأية ١الأولي
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
لَا أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ
La oqsimu biyawmi alqiyamat

Swahili
 
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!

Ayah  75:2  الأية
وَلَا أُقْسِمُ بِالنَّفْسِ اللَّوَّامَةِ
Wala oqsimu binnafsi allawwamat

Swahili
 
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!

Ayah  75:3  الأية
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُ
Ayahsabu al-insanu allannajmaAAa AAithamah

Swahili
 
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?

Ayah  75:4  الأية
بَلَىٰ قَادِرِينَ عَلَىٰ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُ
Bala qadireena AAala annusawwiya bananah

Swahili
 
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!

Ayah  75:5  الأية
بَلْ يُرِيدُ الْإِنسَانُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُ
Bal yureedu al-insanu liyafjura amamah

Swahili
 
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.

Ayah  75:6  الأية
يَسْأَلُ أَيَّانَ يَوْمُ الْقِيَامَةِ
Yas-alu ayyana yawmu alqiyama

Swahili
 
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?

Ayah  75:7  الأية
فَإِذَا بَرِقَ الْبَصَرُ
Fa-itha bariqa albasar

Swahili
 
Basi jicho litapo dawaa,

Ayah  75:8  الأية
وَخَسَفَ الْقَمَرُ
Wakhasafa alqamar

Swahili
 
Na mwezi utapo patwa,

Ayah  75:9  الأية
وَجُمِعَ الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ
WajumiAAa ashshamsu walqamar

Swahili
 
Na likakusanywa jua na mwezi,

Ayah  75:10  الأية
يَقُولُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ الْمَفَرُّ
Yaqoolu al-insanu yawma-ithinayna almafar

Swahili
 
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?

Ayah  75:11  الأية
كَلَّا لَا وَزَرَ
Kalla la wazar

Swahili
 
La! Hapana pa kukimbilia!

Ayah  75:12  الأية
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمُسْتَقَرُّ
Ila rabbika yawma-ithinalmustaqar

Swahili
 
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.

Ayah  75:13  الأية
يُنَبَّأُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Yunabbao al-insanu yawma-ithinbima qaddama waakhkhar

Swahili
 
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.

Ayah  75:14  الأية
بَلِ الْإِنسَانُ عَلَىٰ نَفْسِهِ بَصِيرَةٌ
Bali al-insanu AAala nafsihibaseera

Swahili
 
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.

Ayah  75:15  الأية
وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُ
Walaw alqa maAAatheerah

Swahili
 
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.

Ayah  75:16  الأية
لَا تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ
La tuharrik bihi lisanakalitaAAjala bih

Swahili
 
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.

Ayah  75:17  الأية
إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُ وَقُرْآنَهُ
Inna AAalayna jamAAahu waqur-anah

Swahili
 
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.

Ayah  75:18  الأية
فَإِذَا قَرَأْنَاهُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ
Fa-itha qara/nahu fattabiAAqur-anah

Swahili
 
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.

Ayah  75:19  الأية
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ
Thumma inna AAalayna bayanah

Swahili
 
Kisha ni juu yetu kuubainisha.

Ayah  75:20  الأية
كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ
Kalla bal tuhibboona alAAajila

Swahili
 
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,

Ayah  75:21  الأية
وَتَذَرُونَ الْآخِرَةَ
Watatharoona al-akhira

Swahili
 
Na mnaacha maisha ya Akhera.

Ayah  75:22  الأية
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاضِرَةٌ
Wujoohun yawma-ithin nadira

Swahili
 
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,

Ayah  75:23  الأية
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌ
Ila rabbiha nathira

Swahili
 
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.

Ayah  75:24  الأية
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ بَاسِرَةٌ
Wawujoohun yawma-ithin basira

Swahili
 
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.

Ayah  75:25  الأية
تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌ
Tathunnu an yufAAala bihafaqira

Swahili
 
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.

Ayah  75:26  الأية
كَلَّا إِذَا بَلَغَتِ التَّرَاقِيَ
Kalla itha balaghati attaraqiy

Swahili
 
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,

Ayah  75:27  الأية
وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍ
Waqeela man raq

Swahili
 
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?

Ayah  75:28  الأية
وَظَنَّ أَنَّهُ الْفِرَاقُ
Wathanna annahu alfiraq

Swahili
 
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;

Ayah  75:29  الأية
وَالْتَفَّتِ السَّاقُ بِالسَّاقِ
Waltaffati assaqu bilssaq

Swahili
 
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,

Ayah  75:30  الأية
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمَسَاقُ
Ila rabbika yawma-ithin almasaq

Swahili
 
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!

Ayah  75:31  الأية
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Fala saddaqa wala salla

Swahili
 
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.

Ayah  75:32  الأية
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Walakin kaththaba watawalla

Swahili
 
Bali alikanusha, na akageuka.

Ayah  75:33  الأية
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰ أَهْلِهِ يَتَمَطَّىٰ
Thumma thahaba ila ahlihiyatamatta

Swahili
 
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.

Ayah  75:34  الأية
أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ
Awla laka faawla

Swahili
 
Ole wako, ole wako!

Ayah  75:35  الأية
ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ
Thumma awla laka faawla

Swahili
 
Kisha Ole wako, ole wako!

Ayah  75:36  الأية
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَن يُتْرَكَ سُدًى
Ayahsabu al-insanu an yutrakasuda

Swahili
 
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?

Ayah  75:37  الأية
أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِّن مَّنِيٍّ يُمْنَىٰ
Alam yaku nutfatan min manayyin yumna

Swahili
 
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?

Ayah  75:38  الأية
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
Thumma kana AAalaqatan fakhalaqafasawwa

Swahili
 
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.

Ayah  75:39  الأية
فَجَعَلَ مِنْهُ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ
FajaAAala minhu azzawjayni aththakarawal-ontha

Swahili
 
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.

Ayah  75:40  الأية
أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ
Alaysa thalika biqadirin AAalaan yuhyiya almawta

Swahili
 
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us