1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ
AAabasa watawalla
Swahili
Alikunja kipaji na akageuka,
|
Ayah 80:2 الأية
أَن جَاءَهُ الْأَعْمَىٰ
An jaahu al-aAAma
Swahili
Kwa sababu alimjia kipofu!
|
Ayah 80:3 الأية
وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُ يَزَّكَّىٰ
Wama yudreeka laAAallahu yazzakka
Swahili
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
|
Ayah 80:4 الأية
أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ الذِّكْرَىٰ
Aw yaththakkaru fatanfaAAahu aththikra
Swahili
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
|
Ayah 80:5 الأية
أَمَّا مَنِ اسْتَغْنَىٰ
Amma mani istaghna
Swahili
Ama ajionaye hana haja,
|
Ayah 80:6 الأية
فَأَنتَ لَهُ تَصَدَّىٰ
Faanta lahu tasadda
Swahili
Wewe ndio unamshughulikia?
|
Ayah 80:7 الأية
وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ
Wama AAalayka alla yazzakka
Swahili
Na si juu yako kama hakutakasika.
|
Ayah 80:8 الأية
وَأَمَّا مَن جَاءَكَ يَسْعَىٰ
Waamma man jaaka yasAAa
Swahili
Ama anaye kujia kwa juhudi,
|
Ayah 80:9 الأية
وَهُوَ يَخْشَىٰ
Wahuwa yakhsha
Swahili
Naye anaogopa,
|
Ayah 80:10 الأية
فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ
Faanta AAanhu talahha
Swahili
Ndio wewe unampuuza?
|
Ayah 80:11 الأية
كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ
Kalla innaha tathkira
Swahili
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
|
Ayah 80:12 الأية
فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ
Faman shaa thakarah
Swahili
Basi anaye penda akumbuke.
|
Ayah 80:13 الأية
فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ
Fee suhufin mukarrama
Swahili
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
|
Ayah 80:14 الأية
مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ
MarfooAAatin mutahhara
Swahili
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
|
Ayah 80:15 الأية
بِأَيْدِي سَفَرَةٍ
Bi-aydee safara
Swahili
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
|
Ayah 80:16 الأية
كِرَامٍ بَرَرَةٍ
Kiramin barara
Swahili
Watukufu, wema.
|
Ayah 80:17 الأية
قُتِلَ الْإِنسَانُ مَا أَكْفَرَهُ
Qutila al-insanu ma akfarah
Swahili
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
|
Ayah 80:18 الأية
مِنْ أَيِّ شَيْءٍ خَلَقَهُ
Min ayyi shay-in khalaqah
Swahili
Kwa kitu gani amemuumba?
|
Ayah 80:19 الأية
مِن نُّطْفَةٍ خَلَقَهُ فَقَدَّرَهُ
Min nutfatin khalaqahu faqaddarah
Swahili
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
|
Ayah 80:20 الأية
ثُمَّ السَّبِيلَ يَسَّرَهُ
Thumma assabeela yassarah
Swahili
Kisha akamsahilishia njia.
|
Ayah 80:21 الأية
ثُمَّ أَمَاتَهُ فَأَقْبَرَهُ
Thumma amatahu faaqbarah
Swahili
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
|
Ayah 80:22 الأية
ثُمَّ إِذَا شَاءَ أَنشَرَهُ
Thumma itha shaa ansharah
Swahili
Kisha apendapo atamfufua.
|
Ayah 80:23 الأية
كَلَّا لَمَّا يَقْضِ مَا أَمَرَهُ
Kalla lamma yaqdi maamarah
Swahili
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
|
Ayah 80:24 الأية
فَلْيَنظُرِ الْإِنسَانُ إِلَىٰ طَعَامِهِ
Falyanthuri al-insanuila taAAamih
Swahili
Hebu mtu na atazame chakula chake.
|
Ayah 80:25 الأية
أَنَّا صَبَبْنَا الْمَاءَ صَبًّا
Anna sababna almaasabba
Swahili
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
|
Ayah 80:26 الأية
ثُمَّ شَقَقْنَا الْأَرْضَ شَقًّا
Thumma shaqaqna al-arda shaqqa
Swahili
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
|
Ayah 80:27 الأية
فَأَنبَتْنَا فِيهَا حَبًّا
Faanbatna feeha habba
Swahili
Kisha tukaotesha humo nafaka,
|
Ayah 80:28 الأية
وَعِنَبًا وَقَضْبًا
WaAAinaban waqadba
Swahili
Na zabibu, na mimea ya majani,
|
Ayah 80:29 الأية
وَزَيْتُونًا وَنَخْلًا
Wazaytoonan wanakhla
Swahili
Na mizaituni, na mitende,
|
Ayah 80:30 الأية
وَحَدَائِقَ غُلْبًا
Wahada-iqa ghulba
Swahili
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
|
Ayah 80:31 الأية
وَفَاكِهَةً وَأَبًّا
Wafakihatan waabba
Swahili
Na matunda, na malisho ya wanyama;
|
Ayah 80:32 الأية
مَّتَاعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ
MataAAan lakum wali-anAAamikum
Swahili
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
|
Ayah 80:33 الأية
فَإِذَا جَاءَتِ الصَّاخَّةُ
Fa-itha jaati assakhkha
Swahili
Basi utakapo kuja ukelele,
|
Ayah 80:34 الأية
يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ
Yawma yafirru almaro min akheeh
Swahili
Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye,
|
Ayah 80:35 الأية
وَأُمِّهِ وَأَبِيهِ
Waommihi waabeeh
Swahili
Na mamaye na babaye,
|
Ayah 80:36 الأية
وَصَاحِبَتِهِ وَبَنِيهِ
Wasahibatihi wabaneeh
Swahili
Na mkewe na wanawe -
|
Ayah 80:37 الأية
لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ
Likulli imri-in minhum yawma-ithinsha/nun yughneeh
Swahili
Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.
|
Ayah 80:38 الأية
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ مُّسْفِرَةٌ
Wujoohun yawma-ithin musfira
Swahili
Siku hiyo ziko nyuso zitazo nawiri,
|
Ayah 80:39 الأية
ضَاحِكَةٌ مُّسْتَبْشِرَةٌ
Dahikatun mustabshira
Swahili
Zitacheka, zitachangamka;
|
Ayah 80:40 الأية
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ عَلَيْهَا غَبَرَةٌ
Wawujoohun yawma-ithin AAalayhaghabara
Swahili
Na nyuso siku hiyo zitakuwa na mavumbi,
|
Ayah 80:41 الأية
تَرْهَقُهَا قَتَرَةٌ
Tarhaquha qatara
Swahili
Giza totoro litazifunika,
|
Ayah 80:42 الأية
أُولَٰئِكَ هُمُ الْكَفَرَةُ الْفَجَرَةُ
Ola-ika humu alkafaratu alfajara
Swahili
Hao ndio makafiri watenda maovu.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|