1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
سُورَةٌ أَنزَلْنَاهَا وَفَرَضْنَاهَا وَأَنزَلْنَا فِيهَا آيَاتٍ بَيِّنَاتٍ
لَّعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
Sooratun anzalnaha wafaradnahawaanzalna feeha ayatin bayyinatinlaAAallakum
tathakkaroon
Swahili
HII NI SURA Tuliyo iteremsha na tukailazimisha; tukateremsha ndani yake Aya
zilizo wazi ili mkumbuke.
|
Ayah 24:2 الأية
الزَّانِيَةُ وَالزَّانِي فَاجْلِدُوا كُلَّ وَاحِدٍ مِّنْهُمَا مِائَةَ جَلْدَةٍ ۖ
وَلَا تَأْخُذْكُم بِهِمَا رَأْفَةٌ فِي دِينِ اللهِ إِن كُنتُمْ تُؤْمِنُونَ
بِاللهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ۖ وَلْيَشْهَدْ عَذَابَهُمَا طَائِفَةٌ مِّنَ
الْمُؤْمِنِينَ
Azzaniyatu wazzaneefajlidoo kulla wahidin minhuma mi-atajaldatin wala
ta/khuthkum bihima ra/fatunfee deeni Allahi in kuntum tu/minoona billahiwalyawmi
al-akhiri walyashhad AAathabahumata-ifatun mina almu/mineen
Swahili
Mzinifu mwanamke na mzinifu mwanamume, mtandikeni kila mmoja katika wao bakora
mia. Wala isikushikeni huruma kwa ajili yao katika hukumu ya Mwenyezi Mungu,
ikiwa nyinyi mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Na lishuhudie adhabu
yao kundi la Waumini.
|
Ayah 24:3 الأية
الزَّانِي لَا يَنكِحُ إِلَّا زَانِيَةً أَوْ مُشْرِكَةً وَالزَّانِيَةُ لَا
يَنكِحُهَا إِلَّا زَانٍ أَوْ مُشْرِكٌ ۚ وَحُرِّمَ ذَٰلِكَ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ
Azzanee la yankihuilla zaniyatan aw mushrikatan wazzaniyatula yankihuha illa
zanin awmushrikun wahurrima thalika AAalaalmu/mineen
Swahili
Mwanamume mzinifu hamwoi ila mwanamke mzinifu au mwanamke mshirikina. Na
mwanamke mzinifu haolewi ila na mwanamume mzinifu au mshirikina. Na hayo
yameharimishwa kwa Waumini.
|
Ayah 24:4 الأية
وَالَّذِينَ يَرْمُونَ الْمُحْصَنَاتِ ثُمَّ لَمْ يَأْتُوا بِأَرْبَعَةِ شُهَدَاءَ
فَاجْلِدُوهُمْ ثَمَانِينَ جَلْدَةً وَلَا تَقْبَلُوا لَهُمْ شَهَادَةً أَبَدًا ۚ
وَأُولَٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ
Wallatheena yarmoona almuhsanatithumma lam ya/too bi-arbaAAati shuhadaa
fajlidoohumthamaneena jaldatan wala taqbaloo lahum shahadatanabadan waola-ika
humu alfasiqoon
Swahili
Na wanao wasingizia wanawake mahashumu, kisha wasilete mashahidi wane, basi
watandikeni bakora thamanini, na msiwakubalie ushahidi wao tena. Na hao ndio
wapotovu.
|
Ayah 24:5 الأية
إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ وَأَصْلَحُوا فَإِنَّ اللهَ غَفُورٌ
رَّحِيمٌ
Illa allatheena taboomin baAAdi thalika waaslahoo fa-inna Allahaghafoorun raheem
Swahili
Isipo kuwa wale walio tubu baada ya hayo na wakatengenea; kwani bila ya shaka
Mwenyezi Mungu ni Msamehevu, Mwenye kurehemu.
|
Ayah 24:6 الأية
وَالَّذِينَ يَرْمُونَ أَزْوَاجَهُمْ وَلَمْ يَكُن لَّهُمْ شُهَدَاءُ إِلَّا
أَنفُسُهُمْ فَشَهَادَةُ أَحَدِهِمْ أَرْبَعُ شَهَادَاتٍ بِاللهِ ۙ إِنَّهُ
لَمِنَ الصَّادِقِينَ
Wallatheena yarmoona azwajahumwalam yakun lahum shuhadao illa anfusuhum
fashahadatuahadihim arbaAAu shahadatin billahiinnahu lamina assadiqeen
Swahili
Na wale wanao wasingizia wake zao na hawana mashahidi ila nafsi zao, basi
ushahidi wa mmoja wao utakuwa kushuhudilia mara nne kwa kiapo cha Mwenyezi Mungu
ya kwamba hakika yeye ni katika wasema kweli.
|
Ayah 24:7 الأية
وَالْخَامِسَةُ أَنَّ لَعْنَتَ اللهِ عَلَيْهِ إِن كَانَ مِنَ الْكَاذِبِينَ
Walkhamisatu anna laAAnata AllahiAAalayhi in kana mina alkathibeen
Swahili
Na mara ya tano kwamba laana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake ikiwa ni miongoni
mwa waongo.
|
Ayah 24:8 الأية
وَيَدْرَأُ عَنْهَا الْعَذَابَ أَن تَشْهَدَ أَرْبَعَ شَهَادَاتٍ بِاللهِ ۙ
إِنَّهُ لَمِنَ الْكَاذِبِينَ
Wayadrao AAanha alAAathaba antashhada arbaAAa shahadatin billahiinnahu lamina
alkathibeen
Swahili
Na mke itamwondokea adhabu kwa kutoa shahada mara nne kwa kiapo cha Mwenyezi
Mungu ya kwamba huyu mume ni miongoni mwa waongo.
|
Ayah 24:9 الأية
وَالْخَامِسَةَ أَنَّ غَضَبَ اللهِ عَلَيْهَا إِن كَانَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Walkhamisata anna ghadabaAllahi AAalayha in kana mina assadiqeen
Swahili
Na mara ya tano ya kwamba ghadhabu ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake kama mumewe yu
miongoni mwa wanao sema kweli.
|
Ayah 24:10 الأية
وَلَوْلَا فَضْلُ اللهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ وَأَنَّ اللهَ تَوَّابٌ
حَكِيمٌ
Walawla fadlu AllahiAAalaykum warahmatuhu waanna Allaha tawwabunhakeem
Swahili
Na lau kuwa si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yenu na rehema yake, na ya kuwa
Mwenyezi Mungu ni Mpokeaji toba....
|
Ayah 24:11 الأية
إِنَّ الَّذِينَ جَاءُوا بِالْإِفْكِ عُصْبَةٌ مِّنكُمْ ۚ لَا تَحْسَبُوهُ شَرًّا
لَّكُم ۖ بَلْ هُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۚ لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُم مَّا اكْتَسَبَ مِنَ
الْإِثْمِ ۚ وَالَّذِي تَوَلَّىٰ كِبْرَهُ مِنْهُمْ لَهُ عَذَابٌ عَظِيمٌ
Inna allatheena jaoo bil-ifkiAAusbatun minkum la tahsaboohu sharran lakumbal
huwa khayrun lakum likulli imri-in minhum ma iktasabamina al-ithmi wallathee
tawalla kibrahuminhum lahu AAathabun AAatheem
Swahili
Hakika wale walio leta uwongo ni kundi miongoni mwenu. Msifikiri ni shari kwenu,
bali hiyo ni kheri kwenu. Kila mtu katika wao atapata aliyo yachuma katika
madhambi. Na yule aliyejitwika sehemu yake kubwa miongoni mwao, atapata adhabu
kubwa.
|
Ayah 24:12 الأية
لَّوْلَا إِذْ سَمِعْتُمُوهُ ظَنَّ الْمُؤْمِنُونَ وَالْمُؤْمِنَاتُ بِأَنفُسِهِمْ
خَيْرًا وَقَالُوا هَٰذَا إِفْكٌ مُّبِينٌ
Lawla ith samiAAtumoohu thannaalmu/minoona walmu/minatu bi-anfusihim khayran
waqaloohatha ifkun mubeen
Swahili
Kwa nini mlipo sikia khabari hii, wanaume Waumini na wanawake Waumini
hawakuwadhania wenzao mema, na kusema: Huu ni uzushi dhaahiri?
|
Ayah 24:13 الأية
لَّوْلَا جَاءُوا عَلَيْهِ بِأَرْبَعَةِ شُهَدَاءَ ۚ فَإِذْ لَمْ يَأْتُوا
بِالشُّهَدَاءِ فَأُولَٰئِكَ عِندَ اللهِ هُمُ الْكَاذِبُونَ
Lawla jaoo AAalayhibi-arbaAAati shuhadaa fa-ith lam ya/too
bishshuhada-ifaola-ika AAinda Allahi humu alkathiboon
Swahili
Kwa nini hawakuleta mashahidi wane? Na ilivyo kuwa hawakuleta mashahidi wane
basi hao mbele ya Mwenyezi Mungu ni waongo.
|
Ayah 24:14 الأية
وَلَوْلَا فَضْلُ اللهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ
لَمَسَّكُمْ فِي مَا أَفَضْتُمْ فِيهِ عَذَابٌ عَظِيمٌ
Walawla fadlu AllahiAAalaykum warahmatuhu fee addunya wal-akhiratilamassakum fee
ma afadtum feehi AAathabunAAatheem
Swahili
Na lau kuwa si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yenu na rehema yake katika dunia na
Akhera, bila ya shaka ingeli kupateni adhabu kubwa kwa sababu ya yale mliyo
jiingiza.
|
Ayah 24:15 الأية
إِذْ تَلَقَّوْنَهُ بِأَلْسِنَتِكُمْ وَتَقُولُونَ بِأَفْوَاهِكُم مَّا لَيْسَ
لَكُم بِهِ عِلْمٌ وَتَحْسَبُونَهُ هَيِّنًا وَهُوَ عِندَ اللهِ عَظِيمٌ
Ith talaqqawnahu bi-alsinatikumwataqooloona bi-afwahikum ma laysa lakum
bihiAAilmun watahsaboonahu hayyinan wahuwa AAinda AllahiAAatheem
Swahili
Mlipo yapokea kwa ndimi zenu na mkasema kwa vinywa vyenu msiyo yajua, na
mlifikiri ni jambo dogo, kumbe mbele ya Mwenyezi Mungu ni kubwa.
|
Ayah 24:16 الأية
وَلَوْلَا إِذْ سَمِعْتُمُوهُ قُلْتُم مَّا يَكُونُ لَنَا أَن نَّتَكَلَّمَ
بِهَٰذَا سُبْحَانَكَ هَٰذَا بُهْتَانٌ عَظِيمٌ
Walawla ith samiAAtumoohuqultum ma yakoonu lana an natakallama bihathasubhanaka
hatha buhtanun AAatheem
Swahili
Na kwa nini mlipo yasikia msiseme: Haitufalii kuzungumza haya. Subhanak
Umetakasika! Huu ni uzushi mkubwa!
|
Ayah 24:17 الأية
يَعِظُكُمُ اللهُ أَن تَعُودُوا لِمِثْلِهِ أَبَدًا إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ
YaAAithukumu Allahu antaAAoodoo limithlihi abadan in kuntum mu/mineen
Swahili
Mwenyezi Mungu anakuonyeni msirejee tena kufanya kama haya kabisa, ikiwa nyinyi
ni Waumini!
|
Ayah 24:18 الأية
وَيُبَيِّنُ اللهُ لَكُمُ الْآيَاتِ ۚ وَاللهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Wayubayyinu Allahu lakumu al-ayatiwallahu AAaleemun hakeem
Swahili
Na Mwenyezi Mungu anakubainisheni Aya. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye hikima.
|
Ayah 24:19 الأية
إِنَّ الَّذِينَ يُحِبُّونَ أَن تَشِيعَ الْفَاحِشَةُ فِي الَّذِينَ آمَنُوا لَهُمْ
عَذَابٌ أَلِيمٌ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ ۚ وَاللهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا
تَعْلَمُونَ
Inna allatheena yuhibboona antasheeAAa alfahishatu fee allatheena amanoolahum
AAathabun aleemun fee addunya wal-akhiratiwallahu yaAAlamu waantum la taAAlamoon
Swahili
Kwa hakika wale wanao penda uenee uchafu kwa walio amini, watapata adhabu chungu
katika dunia na Akhera. Na Mwenyezi Mungu anajua na nyinyi hamjui.
|
Ayah 24:20 الأية
وَلَوْلَا فَضْلُ اللهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ وَأَنَّ اللهَ رَءُوفٌ
رَّحِيمٌ
Walawla fadlu AllahiAAalaykum warahmatuhu waanna Allaha raoofun raheem
Swahili
Na lau kuwa si fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yenu na rehema yake, na kuwa hakika
Mwenyezi Mungu ni Mpole, Mwenye kurehemu....
|
Ayah 24:21 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّبِعُوا خُطُوَاتِ الشَّيْطَانِ ۚ وَمَن
يَتَّبِعْ خُطُوَاتِ الشَّيْطَانِ فَإِنَّهُ يَأْمُرُ بِالْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ
ۚ وَلَوْلَا فَضْلُ اللهِ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَتُهُ مَا زَكَىٰ مِنكُم مِّنْ
أَحَدٍ أَبَدًا وَلَٰكِنَّ اللهَ يُزَكِّي مَن يَشَاءُ ۗ وَاللهُ سَمِيعٌ
عَلِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanoola tattabiAAoo khutuwati ashshaytaniwaman yattabiAA
khutuwati ashshaytanifa-innahu ya/muru bilfahsha-i walmunkariwalawla fadlu
Allahi AAalaykum warahmatuhuma zaka minkum min ahadin abadan walakinnaAllaha
yuzakkee man yashao wallahusameeAAun AAaleem
Swahili
Enyi mlio amini! Msizifuate nyayo za Shet'ani. Na atakaye fuata nyayo za
Shet'ani basi yeye huamrisha machafu na maovu. Na lau kuwa si fadhila ya
Mwenyezi Mungu na rehema yake juu yenu, asingeli takasika miongoni mwenu kabisa
hata mmoja. Lakini Mwenyezi Mungu humtakasa amtakaye, na Mwenyezi Mungu ni
Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
|
Ayah 24:22 الأية
وَلَا يَأْتَلِ أُولُو الْفَضْلِ مِنكُمْ وَالسَّعَةِ أَن يُؤْتُوا أُولِي
الْقُرْبَىٰ وَالْمَسَاكِينَ وَالْمُهَاجِرِينَ فِي سَبِيلِ اللهِ ۖ وَلْيَعْفُوا
وَلْيَصْفَحُوا ۗ أَلَا تُحِبُّونَ أَن يَغْفِرَ اللهُ لَكُمْ ۗ وَاللهُ
غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Wala ya/tali oloo alfadliminkum wassaAAati an yu/too olee alqurba
walmasakeenawalmuhajireena fee sabeeli AllahiwalyaAAfoo walyasfahoo ala
tuhibboonaan yaghfira Allahu lakum wallahu ghafoorunraheem
Swahili
Na wale katika nyinyi wenye fadhila na wasaa wasiape kutowapa jamaa zao na
masikini na walio hama kwa Njia ya Mwenyezi Mungu. Na wasamehe, na waachilie
mbali. Je! Nyinyi hampendi Mwenyezi Mungu akusameheni? Na Mwenyezi Mungu ni
Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
|
Ayah 24:23 الأية
إِنَّ الَّذِينَ يَرْمُونَ الْمُحْصَنَاتِ الْغَافِلَاتِ الْمُؤْمِنَاتِ لُعِنُوا
فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ وَلَهُمْ عَذَابٌ عَظِيمٌ
Inna allatheena yarmoona almuhsanatialghafilati almu/minati luAAinoo fee
addunyawal-akhirati walahum AAathabun AAatheem
Swahili
Hakika wanao wasingizia wanawake, wanao jihishimu, walio ghafilika, Waumini,
wamelaaniwa duniani na Akhera, nao watapata adhabu kubwa.
|
Ayah 24:24 الأية
يَوْمَ تَشْهَدُ عَلَيْهِمْ أَلْسِنَتُهُمْ وَأَيْدِيهِمْ وَأَرْجُلُهُم بِمَا
كَانُوا يَعْمَلُونَ
Yawma tashhadu AAalayhim alsinatuhumwaaydeehim waarjuluhum bima kanoo yaAAmaloon
Swahili
Siku ambayo zitawashuhudia ndimi zao na mikono yao na miguu yao kwa waliyo kuwa
wakiyatenda.
|
Ayah 24:25 الأية
يَوْمَئِذٍ يُوَفِّيهِمُ اللهُ دِينَهُمُ الْحَقَّ وَيَعْلَمُونَ أَنَّ اللهَ
هُوَ الْحَقُّ الْمُبِينُ
Yawma-ithin yuwaffeehimu Allahudeenahumu alhaqqa wayaAAlamoona anna Allaha huwa
alhaqqualmubeen
Swahili
Siku hiyo Mwenyezi Mungu atawapa sawa sawa malipo yao ya haki, na watajua kwamba
hakika Mwenyezi Mungu ndiye Haki Iliyo Wazi.
|
Ayah 24:26 الأية
الْخَبِيثَاتُ لِلْخَبِيثِينَ وَالْخَبِيثُونَ لِلْخَبِيثَاتِ ۖ وَالطَّيِّبَاتُ
لِلطَّيِّبِينَ وَالطَّيِّبُونَ لِلطَّيِّبَاتِ ۚ أُولَٰئِكَ مُبَرَّءُونَ مِمَّا
يَقُولُونَ ۖ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَرِزْقٌ كَرِيمٌ
Alkhabeethatu lilkhabeetheena walkhabeethoonalilkhabeethati wattayyibatu
littayyibeenawattayyiboona littayyibatiola-ika mubarraoona mimma yaqooloona
lahummaghfiratun warizqun kareem
Swahili
Wanawake waovu ni wa wanaume waovu, na wanaume waovu ni wa wanawake waovu. Na
wanawake wema ni wa wanaume wema, na wanaume wema ni wa wanawake wema. Hao
wameepushwa na hayo wanayo yasema; wao watapata msamaha na riziki ya ukarimu.
|
Ayah 24:27 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَدْخُلُوا بُيُوتًا غَيْرَ بُيُوتِكُمْ
حَتَّىٰ تَسْتَأْنِسُوا وَتُسَلِّمُوا عَلَىٰ أَهْلِهَا ۚ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ
لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
Ya ayyuha allatheena amanoola tadkhuloo buyootan ghayra buyootikum
hattatasta/nisoo watusallimoo AAala ahliha thalikumkhayrun lakum laAAallakum
tathakkaroon
Swahili
Enyi mlio amini! Msiingie nyumba zisio nyumba zenu mpaka mwombe ruhusa, na
mwatolee salamu wenyewe. Hayo ni bora kwenu mpate kukumbuka.
|
Ayah 24:28 الأية
فَإِن لَّمْ تَجِدُوا فِيهَا أَحَدًا فَلَا تَدْخُلُوهَا حَتَّىٰ يُؤْذَنَ لَكُمْ ۖ
وَإِن قِيلَ لَكُمُ ارْجِعُوا فَارْجِعُوا ۖ هُوَ أَزْكَىٰ لَكُمْ ۚ وَاللهُ
بِمَا تَعْمَلُونَ عَلِيمٌ
Fa-in lam tajidoo feeha ahadanfala tadkhulooha hatta yu/thanalakum wa-in qeela
lakumu irjiAAoo farjiAAoo huwa azkalakum wallahu bima taAAmaloona AAaleem
Swahili
Na msipo mkuta mtu humo basi msiingie mpaka mruhusiwe. Na mkiambiwa: Rudini!
Basi rudini. Hivi ni usafi zaidi kwenu. Na Mwenyezi Mungu anajua mnayo yatenda.
|
Ayah 24:29 الأية
لَّيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَدْخُلُوا بُيُوتًا غَيْرَ مَسْكُونَةٍ فِيهَا
مَتَاعٌ لَّكُمْ ۚ وَاللهُ يَعْلَمُ مَا تُبْدُونَ وَمَا تَكْتُمُونَ
Laysa AAalaykum junahun an tadkhuloobuyootan ghayra maskoonatin feeha mataAAun
lakum wallahuyaAAlamu ma tubdoona wama taktumoon
Swahili
Si vibaya kwenu kuingia nyumba zisio kaliwa ambazo ndani yake yamo manufaa yenu.
Na Mwenyezi Mungu anajua mnayo yadhihirisha na mnayo yaficha.
|
Ayah 24:30 الأية
قُل لِّلْمُؤْمِنِينَ يَغُضُّوا مِنْ أَبْصَارِهِمْ وَيَحْفَظُوا فُرُوجَهُمْ ۚ
ذَٰلِكَ أَزْكَىٰ لَهُمْ ۗ إِنَّ اللهَ خَبِيرٌ بِمَا يَصْنَعُونَ
Qul lilmu/mineena yaghuddoo min absarihumwayahfathoo furoojahum thalika
azkalahum inna Allaha khabeerun bima yasnaAAoon
Swahili
Waambie Waumini wanaume wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao. Hili ni
takaso bora kwao. Hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za wanayo yafanya.
|
Ayah 24:31 الأية
وَقُل لِّلْمُؤْمِنَاتِ يَغْضُضْنَ مِنْ أَبْصَارِهِنَّ وَيَحْفَظْنَ فُرُوجَهُنَّ
وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ۖ وَلْيَضْرِبْنَ
بِخُمُرِهِنَّ عَلَىٰ جُيُوبِهِنَّ ۖ وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا
لِبُعُولَتِهِنَّ أَوْ آبَائِهِنَّ أَوْ آبَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ أَبْنَائِهِنَّ
أَوْ أَبْنَاءِ بُعُولَتِهِنَّ أَوْ إِخْوَانِهِنَّ أَوْ بَنِي إِخْوَانِهِنَّ أَوْ
بَنِي أَخَوَاتِهِنَّ أَوْ نِسَائِهِنَّ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ أَوِ
التَّابِعِينَ غَيْرِ أُولِي الْإِرْبَةِ مِنَ الرِّجَالِ أَوِ الطِّفْلِ الَّذِينَ
لَمْ يَظْهَرُوا عَلَىٰ عَوْرَاتِ النِّسَاءِ ۖ وَلَا يَضْرِبْنَ بِأَرْجُلِهِنَّ
لِيُعْلَمَ مَا يُخْفِينَ مِن زِينَتِهِنَّ ۚ وَتُوبُوا إِلَى اللهِ جَمِيعًا
أَيُّهَ الْمُؤْمِنُونَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ
Waqul lilmu/minati yaghdudnamin absarihinna wayahfathnafuroojahunna wala
yubdeena zeenatahunna illa mathahara minha walyadribnabikhumurihinna AAala
juyoobihinna wala yubdeenazeenatahunna illa libuAAoolatihinna aw aba-ihinnaaw
aba-i buAAoolatihinna aw abna-ihinna awabna-i buAAoolatihinna aw ikhwanihinna aw
baneeikhwanihinna aw banee akhawatihinna aw nisa-ihinnaaw ma malakat aymanuhunna
awi attabiAAeenaghayri olee al-irbati mina arrijali awi attifliallatheena lam
yathharoo AAala AAawratiannisa-i wala yadribnabi-arjulihinna liyuAAlama ma
yukhfeena min zeenatihinnawatooboo ila Allahi jameeAAan ayyuhaalmu/minoona
laAAallakum tuflihoon
Swahili
Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao, na wazilinde tupu zao, wala
wasionyeshe uzuri wao isipo kuwa unao dhihirika. Na waangushe shungi zao juu ya
vifua vyao, wala wasionyeshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao, au baba
wa waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao, au kaka zao, au wana wa
kaka zao, au wana wa dada zao, au wanawake wenzao, au iliyo wamiliki mikono yao
ya kuume, au wafwasi wanaume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo
yaliyo khusu uke. Wala wasipige chini miguu yao ili yajuulikane mapambo waliyo
yaficha. Na tubuni nyote kwa Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa.
|
Ayah 24:32 الأية
وَأَنكِحُوا الْأَيَامَىٰ مِنكُمْ وَالصَّالِحِينَ مِنْ عِبَادِكُمْ وَإِمَائِكُمْ
ۚ إِن يَكُونُوا فُقَرَاءَ يُغْنِهِمُ اللهُ مِن فَضْلِهِ ۗ وَاللهُ وَاسِعٌ
عَلِيمٌ
Waankihoo al-ayamaminkum wassaliheena min AAibadikumwa-ima-ikum in yakoonoo
fuqaraa yughnihimu Allahumin fadlihi wallahu wasiAAun AAaleem
Swahili
Na waozeni wajane miongoni mwenu na wema katika watumwa wenu na wajakazi wenu.
Wakiwa mafakiri Mwenyezi Mungu atawatajirisha kwa fadhila yake. Na Mwenyezi
Mungu ni Mwenye wasaa Mwenye kujua.
|
Ayah 24:33 الأية
وَلْيَسْتَعْفِفِ الَّذِينَ لَا يَجِدُونَ نِكَاحًا حَتَّىٰ يُغْنِيَهُمُ اللهُ
مِن فَضْلِهِ ۗ وَالَّذِينَ يَبْتَغُونَ الْكِتَابَ مِمَّا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ
فَكَاتِبُوهُمْ إِنْ عَلِمْتُمْ فِيهِمْ خَيْرًا ۖ وَآتُوهُم مِّن مَّالِ اللهِ
الَّذِي آتَاكُمْ ۚ وَلَا تُكْرِهُوا فَتَيَاتِكُمْ عَلَى الْبِغَاءِ إِنْ أَرَدْنَ
تَحَصُّنًا لِّتَبْتَغُوا عَرَضَ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ۚ وَمَن يُكْرِههُّنَّ
فَإِنَّ اللهَ مِن بَعْدِ إِكْرَاهِهِنَّ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
WalyastaAAfifi allatheena layajidoona nikahan hatta yughniyahumu Allahumin
fadlihi wallatheena yabtaghoona alkitabamimma malakat aymanukum fakatiboohum
inAAalimtum feehim khayran waatoohum min mali Allahiallathee atakum wala
tukrihoo fatayatikumAAala albigha-i in aradna tahassunanlitabtaghoo AAarada
alhayati addunyawaman yukrihhunna fa-inna Allaha min baAAdi ikrahihinnaghafoorun
raheem
Swahili
Na wajizuilie na machafu wale wasio pata cha kuolea, mpaka Mwenyezi Mungu
awatajirishe kwa fadhila yake. Na wanao taka kuandikiwa uhuru katika wale ambao
mikono yenu ya kulia imewamiliki, basi waandikieni kama mkiona wema kwao. Na
wapeni katika mali ya Mwenyezi Mungu aliyo kupeni. Wala msiwashurutishe vijakazi
vyenu kufanya zina kwa ajili ya kutafuta pato la maisha ya dunia, ilhali wao
wanataka kujihishimu. Na atakaye walazimisha basi Mwenyezi Mungu baada ya
kulazimishwa kwao huko, atawasamehe, kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe,
Mwenye kurehemu.
|
Ayah 24:34 الأية
وَلَقَدْ أَنزَلْنَا إِلَيْكُمْ آيَاتٍ مُّبَيِّنَاتٍ وَمَثَلًا مِّنَ الَّذِينَ
خَلَوْا مِن قَبْلِكُمْ وَمَوْعِظَةً لِّلْمُتَّقِينَ
Walaqad anzalna ilaykum ayatinmubayyinatin wamathalan mina allatheena khalaw
minqablikum wamawAAithatan lilmuttaqeen
Swahili
Na kwa yakini tumekuteremshieni Ishara zilizo wazi na mifano kutokana na walio
tangulia kabla yenu na mawaidha kwa wachamngu.
|
Ayah 24:35 الأية
اللهُ نُورُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ مَثَلُ نُورِهِ كَمِشْكَاةٍ فِيهَا
مِصْبَاحٌ ۖ الْمِصْبَاحُ فِي زُجَاجَةٍ ۖ الزُّجَاجَةُ كَأَنَّهَا كَوْكَبٌ
دُرِّيٌّ يُوقَدُ مِن شَجَرَةٍ مُّبَارَكَةٍ زَيْتُونَةٍ لَّا شَرْقِيَّةٍ وَلَا
غَرْبِيَّةٍ يَكَادُ زَيْتُهَا يُضِيءُ وَلَوْ لَمْ تَمْسَسْهُ نَارٌ ۚ نُّورٌ
عَلَىٰ نُورٍ ۗ يَهْدِي اللهُ لِنُورِهِ مَن يَشَاءُ ۚ وَيَضْرِبُ اللهُ
الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ ۗ وَاللهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
Allahu nooru assamawatiwal-ardi mathalu noorihi kamishkatin feehamisbahun
almisbahu fee zujajatinazzujajatu kaannaha kawkabun durriyyunyooqadu min
shajaratin mubarakatin zaytoonatin lasharqiyyatin wala gharbiyyatin yakadu
zaytuhayudee-o walaw lam tamsas-hu narun noorun AAalanoorin yahdee Allahu
linoorihi man yashao wayadribuAllahu al-amthala linnasi wallahubikulli shay-in
AAaleem
Swahili
Mwenyezi Mungu ni Nuru ya Mbingu na Ardhi. Mfano wa Nuru yake ni kama shubaka
lenye kuwekwa ndani yake taa. Taa ile imo katika tungi. Tungi lile ni kama nyota
inayo meremeta, inayo washwa kwa mafuta yanayo toka katika mti ulio barikiwa,
mzaituni. Si wa mashariki wala magharibi. Yanakaribia mafuta yake kung'aa
wenyewe ingawa moto haujayagusa - Nuru juu ya Nuru. Mwenyezi Mungu humwongoa
kwenye Nuru yake amtakaye. Na Mwenyezi Mungu huwapigia watu mifano. Na Mwenyezi
Mungu ni Mwenye kujua kila kitu.
|
Ayah 24:36 الأية
فِي بُيُوتٍ أَذِنَ اللهُ أَن تُرْفَعَ وَيُذْكَرَ فِيهَا اسْمُهُ يُسَبِّحُ لَهُ
فِيهَا بِالْغُدُوِّ وَالْآصَالِ
Fee buyootin athina Allahu anturfaAAa wayuthkara feeha ismuhu yusabbihulahu
feeha bilghuduwwi wal-asal
Swahili
Katika Nyumba ambazo Mwenyezi Mungu ameamrisha zitukuzwe, na humo litajwe jina
lake, wanamtakasa humo asubuhi na jioni
|
Ayah 24:37 الأية
رِجَالٌ لَّا تُلْهِيهِمْ تِجَارَةٌ وَلَا بَيْعٌ عَن ذِكْرِ اللهِ وَإِقَامِ
الصَّلَاةِ وَإِيتَاءِ الزَّكَاةِ ۙ يَخَافُونَ يَوْمًا تَتَقَلَّبُ فِيهِ
الْقُلُوبُ وَالْأَبْصَارُ
Rijalun la tulheehim tijaratunwala bayAAun AAan thikri Allahi wa-iqamiassalati
wa-eeta-i azzakatiyakhafoona yawman tataqallabu feehi alquloobu wal-absar
Swahili
Watu ambao biashara wala kuuza hakuwashughulishi na kumdhukuru Mwenyezi Mungu,
na kushika Sala, na kutoa Zaka. Wanaikhofu Siku ambayo nyoyo na macho yatageuka.
|
Ayah 24:38 الأية
لِيَجْزِيَهُمُ اللهُ أَحْسَنَ مَا عَمِلُوا وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ ۗ
وَاللهُ يَرْزُقُ مَن يَشَاءُ بِغَيْرِ حِسَابٍ
Liyajziyahumu Allahu ahsana maAAamiloo wayazeedahum min fadlihi wallahuyarzuqu
man yashao bighayri hisab
Swahili
Ili Mwenyezi Mungu awalipe bora ya waliyo yatenda, na awazidishie katika fadhila
zake. Na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila ya hisabu.
|
Ayah 24:39 الأية
وَالَّذِينَ كَفَرُوا أَعْمَالُهُمْ كَسَرَابٍ بِقِيعَةٍ يَحْسَبُهُ الظَّمْآنُ
مَاءً حَتَّىٰ إِذَا جَاءَهُ لَمْ يَجِدْهُ شَيْئًا وَوَجَدَ اللهَ عِندَهُ
فَوَفَّاهُ حِسَابَهُ ۗ وَاللهُ سَرِيعُ الْحِسَابِ
Wallatheena kafaroo aAAmaluhumkasarabin biqeeAAatin yahsabuhu aththam-anumaan
hatta itha jaahu lamyajidhu shay-an wawajada Allaha AAindahu fawaffahu
hisabahuwallahu sareeAAu alhisab
Swahili
Na walio kufuru vitendo vyao ni kama sarabi (mazigazi) uwandani. Mwenye kiu
huyadhania ni maji. Hata akiyaendea hapati chochote. Na atamkuta Mwenyezi Mungu
hapo naye amlipe hisabu yake sawa sawa. Na Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa
kuhisabu.
|
Ayah 24:40 الأية
أَوْ كَظُلُمَاتٍ فِي بَحْرٍ لُّجِّيٍّ يَغْشَاهُ مَوْجٌ مِّن فَوْقِهِ مَوْجٌ مِّن
فَوْقِهِ سَحَابٌ ۚ ظُلُمَاتٌ بَعْضُهَا فَوْقَ بَعْضٍ إِذَا أَخْرَجَ يَدَهُ لَمْ
يَكَدْ يَرَاهَا ۗ وَمَن لَّمْ يَجْعَلِ اللهُ لَهُ نُورًا فَمَا لَهُ مِن نُّورٍ
Aw kathulumatin fee bahrinlujjiyyin yaghshahu mawjun min fawqihi mawjun min
fawqihisahabun thulumatun baAAduhafawqa baAAdin itha akhraja yadahu lam yakad
yarahawaman lam yajAAali Allahu lahu nooran fama lahu minnoor
Swahili
Au ni kama giza katika bahari kuu, iliyo funikwa na mawimbi juu ya mawimbi, na
juu yake yapo mawingu. Giza juu ya giza. Akiutoa mtu mkono wake anakaribia
asiuone. Na ambaye Mwenyezi Mungu hakumjaalia kuwa na nuru hawi na nuru.
|
Ayah 24:41 الأية
أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللهَ يُسَبِّحُ لَهُ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ
وَالطَّيْرُ صَافَّاتٍ ۖ كُلٌّ قَدْ عَلِمَ صَلَاتَهُ وَتَسْبِيحَهُ ۗ وَاللهُ
عَلِيمٌ بِمَا يَفْعَلُونَ
Alam tara anna Allaha yusabbihulahu man fee assamawati wal-ardiwattayru saffatin
kullun qadAAalima salatahu watasbeehahu wallahuAAaleemun bima yafAAaloon
Swahili
Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu vinamtakasa vilivyomo katika mbingu na ardhi, na
ndege wakikunjua mbawa zao? Kila mmoja amekwisha jua Sala yake na namna ya
kumtakasa kwake. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuyajua wayatendayo.
|
Ayah 24:42 الأية
وَلِلَّهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ وَإِلَى اللهِ الْمَصِيرُ
Walillahi mulku assamawatiwal-ardi wa-ila Allahi almaseer
Swahili
Na ni wa Mwenyezi Mungu ufalme wa mbingu na ardhi, na kwa Mwenyezi Mungu ndio
marejeo ya wote.
|
Ayah 24:43 الأية
أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللهَ يُزْجِي سَحَابًا ثُمَّ يُؤَلِّفُ بَيْنَهُ ثُمَّ
يَجْعَلُهُ رُكَامًا فَتَرَى الْوَدْقَ يَخْرُجُ مِنْ خِلَالِهِ وَيُنَزِّلُ مِنَ
السَّمَاءِ مِن جِبَالٍ فِيهَا مِن بَرَدٍ فَيُصِيبُ بِهِ مَن يَشَاءُ وَيَصْرِفُهُ
عَن مَّن يَشَاءُ ۖ يَكَادُ سَنَا بَرْقِهِ يَذْهَبُ بِالْأَبْصَارِ
Alam tara anna Allaha yuzjee sahabanthumma yu-allifu baynahu thumma yajAAaluhu
rukaman fataraalwadqa yakhruju min khilalihi wayunazzilu mina assama-imin
jibalin feeha min baradin fayuseebu bihiman yashao wayasrifuhu AAan man yashao
yakadusana barqihi yathhabu bil-absar
Swahili
Je! Huoni ya kwamba Mwenyezi Mungu huyasukuma mawingu, kisha huyaambatisha,
kisha huyafanya mirundi? Basi utaona mvua ikitoka kati yake. Na huteremsha
kutoka juu kwenye milima ya mawingu mvua ya mawe, akamsibu nayo amtakaye na
akamuepusha nayo amtakaye. Hukurubia mmetuko wa umeme wake kupofua macho.
|
Ayah 24:44 الأية
يُقَلِّبُ اللهُ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ ۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبْرَةً
لِّأُولِي الْأَبْصَارِ
Yuqallibu Allahu allayla wannaharainna fee thalika laAAibratan li-olee al-absar
Swahili
Mwenyezi Mungu hubadilisha usiku na mchana. Hakika katika hayo yapo mazingatio
kwa wenye kuona.
|
Ayah 24:45 الأية
وَاللهُ خَلَقَ كُلَّ دَابَّةٍ مِّن مَّاءٍ ۖ فَمِنْهُم مَّن يَمْشِي عَلَىٰ
بَطْنِهِ وَمِنْهُم مَّن يَمْشِي عَلَىٰ رِجْلَيْنِ وَمِنْهُم مَّن يَمْشِي عَلَىٰ
أَرْبَعٍ ۚ يَخْلُقُ اللهُ مَا يَشَاءُ ۚ إِنَّ اللهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ
قَدِيرٌ
Wallahu khalaqa kulla dabbatinmin ma-in faminhum man yamshee AAala
batnihiwaminhum man yamshee AAala rijlayni waminhum man yamsheeAAala arbaAAin
yakhluqu Allahu ma yashaoinna Allaha AAala kulli shay-in qadeer
Swahili
Na Mwenyezi Mungu ameumba kila kinyama kutokana na maji. Wengine katika wao
huenda kwa matumbo yao, na wengine huenda kwa miguu miwili, na wengine huenda
kwa miguu mine. Mwenyezi Mungu huumba ayatakayo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza
wa kila kitu.
|
Ayah 24:46 الأية
لَّقَدْ أَنزَلْنَا آيَاتٍ مُّبَيِّنَاتٍ ۚ وَاللهُ يَهْدِي مَن يَشَاءُ إِلَىٰ
صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ
Laqad anzalna ayatinmubayyinatin wallahu yahdee man yashaoila siratin mustaqeem
Swahili
Kwa yakini tumeteremsha Ishara zinazo bainisha. Na Mwenyezi Mungu hummwongoa
amtakaye kwenye Njia Iliyo Nyooka.
|
Ayah 24:47 الأية
وَيَقُولُونَ آمَنَّا بِاللهِ وَبِالرَّسُولِ وَأَطَعْنَا ثُمَّ يَتَوَلَّىٰ
فَرِيقٌ مِّنْهُم مِّن بَعْدِ ذَٰلِكَ ۚ وَمَا أُولَٰئِكَ بِالْمُؤْمِنِينَ
Wayaqooloona amanna billahiwabirrasooli waataAAna thumma yatawallafareequn
minhum min baAAdi thalika wama ola-ikabilmu/mineen
Swahili
Na wanasema: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na Mtume, na tumet'ii. Kisha kikundi
katika hao hugeuka baada ya hayo. Wala hao si wenye kuamini.
|
Ayah 24:48 الأية
وَإِذَا دُعُوا إِلَى اللهِ وَرَسُولِهِ لِيَحْكُمَ بَيْنَهُمْ إِذَا فَرِيقٌ
مِّنْهُم مُّعْرِضُونَ
Wa-itha duAAoo ila Allahiwarasoolihi liyahkuma baynahum itha fareequn
minhummuAAridoon
Swahili
Na wanapo itwa kumuendea Mwenyezi Mungu na Mtume wake ili ahukumu baina yao,
kipo kikundi katika wao kinakataa.
|
Ayah 24:49 الأية
وَإِن يَكُن لَّهُمُ الْحَقُّ يَأْتُوا إِلَيْهِ مُذْعِنِينَ
Wa-in yakun lahumu alhaqqu ya/tooilayhi muthAAineen
Swahili
Na ikiwa haki ni yao, wanamjia kwa kut'ii.
|
Ayah 24:50 الأية
أَفِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ أَمِ ارْتَابُوا أَمْ يَخَافُونَ أَن يَحِيفَ اللهُ
عَلَيْهِمْ وَرَسُولُهُ ۚ بَلْ أُولَٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ
Afee quloobihim maradun ami irtabooam yakhafoona an yaheefa Allahu
AAalayhimwarasooluhu bal ola-ika humu aththalimoon
Swahili
Je! Wana maradhi katika nyoyo zao, au wanaona shaka, au wanaogopa ya kuwa
Mwenyezi Mungu na Mtume wake watawadhulumu? Bali hao ndio madhaalimu.
|
Ayah 24:51 الأية
إِنَّمَا كَانَ قَوْلَ الْمُؤْمِنِينَ إِذَا دُعُوا إِلَى اللهِ وَرَسُولِهِ
لِيَحْكُمَ بَيْنَهُمْ أَن يَقُولُوا سَمِعْنَا وَأَطَعْنَا ۚ وَأُولَٰئِكَ هُمُ
الْمُفْلِحُونَ
Innama kana qawla almu/mineenaitha duAAoo ila Allahi warasoolihi
liyahkumabaynahum an yaqooloo samiAAna waataAAna waola-ikahumu almuflihoon
Swahili
Haiwi kauli ya Waumini wanapo itwa kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake ili ahukumu
baina yao, ila ni kusema: Tumesikia, na tumet'ii! Na hao ndio wenye kufanikiwa.
|
Ayah 24:52 الأية
وَمَن يُطِعِ اللهَ وَرَسُولَهُ وَيَخْشَ اللهَ وَيَتَّقْهِ فَأُولَٰئِكَ هُمُ
الْفَائِزُونَ
Waman yutiAAi Allahawarasoolahu wayakhsha Allaha wayattaqhi faola-ikahumu
alfa-izoon
Swahili
Na wenye kumt'ii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na wakamwogopa Mwenyezi Mungu na
wakamcha, basi hao ndio wenye kufuzu.
|
Ayah 24:53 الأية
وَأَقْسَمُوا بِاللهِ جَهْدَ أَيْمَانِهِمْ لَئِنْ أَمَرْتَهُمْ لَيَخْرُجُنَّ ۖ
قُل لَّا تُقْسِمُوا ۖ طَاعَةٌ مَّعْرُوفَةٌ ۚ إِنَّ اللهَ خَبِيرٌ بِمَا
تَعْمَلُونَ
Waaqsamoo billahi jahda aymanihimla-in amartahum layakhrujunna qul la tuqsimoo
taAAatunmaAAroofatun inna Allaha khabeerun bima taAAmaloon
Swahili
Na wanaapa kwa Mwenyezi Mungu ukomo wa kiapo chao ya kwamba ukiwaamrisha kwa
yakini watatoka. Sema: Msiape! Ut'iifu unajuulikana. Hakika Mwenyezi Mungu anazo
khabari za mnayo yatenda.
|
Ayah 24:54 الأية
قُلْ أَطِيعُوا اللهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ ۖ فَإِن تَوَلَّوْا فَإِنَّمَا
عَلَيْهِ مَا حُمِّلَ وَعَلَيْكُم مَّا حُمِّلْتُمْ ۖ وَإِن تُطِيعُوهُ تَهْتَدُوا
ۚ وَمَا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ
Qul ateeAAoo Allaha waateeAAooarrasoola fa-in tawallaw fa-innama AAalayhi
mahummila waAAalaykum ma hummiltum wa-in tuteeAAoohutahtadoo wama AAala
arrasooli illaalbalaghu almubeen
Swahili
Sema: Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume. Na mkigeuka, basi yaliyo juu
yake ni aliyo bebeshwa, na yaliyo juu yenu ni mliyo bebshwa nyinyi. Na mkimt'ii
yeye mtaongoka. Na hapana juu ya Mtume ila kufikisha Ujumbe wazi wazi.
|
Ayah 24:55 الأية
وَعَدَ اللهُ الَّذِينَ آمَنُوا مِنكُمْ وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ
لَيَسْتَخْلِفَنَّهُمْ فِي الْأَرْضِ كَمَا اسْتَخْلَفَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ
وَلَيُمَكِّنَنَّ لَهُمْ دِينَهُمُ الَّذِي ارْتَضَىٰ لَهُمْ وَلَيُبَدِّلَنَّهُم
مِّن بَعْدِ خَوْفِهِمْ أَمْنًا ۚ يَعْبُدُونَنِي لَا يُشْرِكُونَ بِي شَيْئًا ۚ
وَمَن كَفَرَ بَعْدَ ذَٰلِكَ فَأُولَٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ
WaAAada Allahu allatheena amanoominkum waAAamiloo assalihatilayastakhlifannahum
fee al-ardi kama istakhlafaallatheena min qablihim walayumakkinanna lahum
deenahumuallathee irtada lahum walayubaddilannahum minbaAAdi khawfihim amnan
yaAAbudoonanee la yushrikoona beeshay-an waman kafara baAAda thalika faola-ika
humualfasiqoon
Swahili
Mwenyezi Mungu amewaahidi wale walio amini miongoni mwenu na wakatenda mema, ya
kwamba atawafanya makhalifa katika ardhi kama alivyo wafanya makhalifa wa kabla
yao, na kwa yakini atawasimamishia Dini yao aliyo wapendelea, na atawabadilishia
amani baada ya khofu yao. Wawe wananiabudu Mimi, wala wasinishirikishe na
chochote. Na watao kufuru baada ya hayo, basi hao ndio wapotovu.
|
Ayah 24:56 الأية
وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ لَعَلَّكُمْ
تُرْحَمُونَ
Waaqeemoo assalata waatooazzakata waateeAAoo arrasoolalaAAallakum turhamoon
Swahili
Na shikeni Sala, na toeni Zaka, na mt'iini Mtume, ili mpate kurehemewa.
|
Ayah 24:57 الأية
لَا تَحْسَبَنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا مُعْجِزِينَ فِي الْأَرْضِ ۚ وَمَأْوَاهُمُ
النَّارُ ۖ وَلَبِئْسَ الْمَصِيرُ
La tahsabanna allatheenakafaroo muAAjizeena fee al-ardi wama/wahumu
annaruwalabi/sa almaseer
Swahili
Msiwadhanie walio kufuru kwamba watashinda katika nchi. Na makaazi yao ni
Motoni, na hakika ni maovu kweli marejeo yao.
|
Ayah 24:58 الأية
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لِيَسْتَأْذِنكُمُ الَّذِينَ مَلَكَتْ
أَيْمَانُكُمْ وَالَّذِينَ لَمْ يَبْلُغُوا الْحُلُمَ مِنكُمْ ثَلَاثَ مَرَّاتٍ ۚ
مِّن قَبْلِ صَلَاةِ الْفَجْرِ وَحِينَ تَضَعُونَ ثِيَابَكُم مِّنَ الظَّهِيرَةِ
وَمِن بَعْدِ صَلَاةِ الْعِشَاءِ ۚ ثَلَاثُ عَوْرَاتٍ لَّكُمْ ۚ لَيْسَ عَلَيْكُمْ
وَلَا عَلَيْهِمْ جُنَاحٌ بَعْدَهُنَّ ۚ طَوَّافُونَ عَلَيْكُم بَعْضُكُمْ عَلَىٰ
بَعْضٍ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللهُ لَكُمُ الْآيَاتِ ۗ وَاللهُ عَلِيمٌ
حَكِيمٌ
Ya ayyuha allatheena amanooliyasta/thinkumu allatheena malakat
aymanukumwallatheena lam yablughoo alhuluma minkumthalatha marratin min qabli
salatialfajri waheena tadaAAoona thiyabakum mina aththaheeratiwamin baAAdi
salati alAAisha-i thalathuAAawratin lakum laysa AAalaykum wala AAalayhim
junahunbaAAdahunna tawwafoona AAalaykum baAAdukumAAala baAAdin kathalika
yubayyinu Allahulakumu al-ayati wallahu AAaleemun hakeem
Swahili
Enyi mlio amini! Nawakutakeni idhini iliyo wamiliki mikono yenu ya kulia na
walio bado kubaalighi miongoni mwenu mara tatu - kabla ya Sala ya alfajiri, na
wakati mnapo vua nguo zenu adhuhuri, na baada ya Sala ya isha. Hizi ni nyakati
tatu za faragha kwenu. Si vibaya kwenu wala kwao baada ya nyakati hizi,
kuzungukiana nyinyi kwa nyinyi. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyo kuelezeni Aya
zake, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye hikima.
|
Ayah 24:59 الأية
وَإِذَا بَلَغَ الْأَطْفَالُ مِنكُمُ الْحُلُمَ فَلْيَسْتَأْذِنُوا كَمَا
اسْتَأْذَنَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللهُ لَكُمْ
آيَاتِهِ ۗ وَاللهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Wa-itha balagha al-atfaluminkumu alhuluma falyasta/thinoo kama
ista/thanaallatheena min qablihim kathalika yubayyinu Allahulakum ayatihi
wallahu AAaleemun hakeem
Swahili
Na watoto wanapo fikilia umri wa kubaalighi basi nawatake ruhusa, kama walivyo
taka ruhusa wa kabla yao. Hivyo ndivyo anavyo kubainishieni Mwenyezi Mungu Aya
zake, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye hikima.
|
Ayah 24:60 الأية
وَالْقَوَاعِدُ مِنَ النِّسَاءِ اللَّاتِي لَا يَرْجُونَ نِكَاحًا فَلَيْسَ
عَلَيْهِنَّ جُنَاحٌ أَن يَضَعْنَ ثِيَابَهُنَّ غَيْرَ مُتَبَرِّجَاتٍ بِزِينَةٍ ۖ
وَأَن يَسْتَعْفِفْنَ خَيْرٌ لَّهُنَّ ۗ وَاللهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ
WalqawaAAidu mina annisa-iallatee la yarjoona nikahan falaysaAAalayhinna junahun
an yadaAAna thiyabahunnaghayra mutabarrijatin bizeenatin waan yastaAAfifna
khayrunlahunna wallahu sameeAAun AAaleem
Swahili
Na wanawake wazee wasio taraji kuolewa, si vibaya kwao kupunguza nguo zao, bila
ya kujishaua kwa mapambo. Na wakijihishimu ni bora kwao. Na Mwenyezi Mungu ni
Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
|
Ayah 24:61 الأية
لَّيْسَ عَلَى الْأَعْمَىٰ حَرَجٌ وَلَا عَلَى الْأَعْرَجِ حَرَجٌ وَلَا عَلَى
الْمَرِيضِ حَرَجٌ وَلَا عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ أَن تَأْكُلُوا مِن بُيُوتِكُمْ أَوْ
بُيُوتِ آبَائِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أُمَّهَاتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ إِخْوَانِكُمْ أَوْ
بُيُوتِ أَخَوَاتِكُمْ أَوْ بُيُوتِ أَعْمَامِكُمْ أَوْ بُيُوتِ عَمَّاتِكُمْ أَوْ
بُيُوتِ أَخْوَالِكُمْ أَوْ بُيُوتِ خَالَاتِكُمْ أَوْ مَا مَلَكْتُم مَّفَاتِحَهُ
أَوْ صَدِيقِكُمْ ۚ لَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَأْكُلُوا جَمِيعًا أَوْ
أَشْتَاتًا ۚ فَإِذَا دَخَلْتُم بُيُوتًا فَسَلِّمُوا عَلَىٰ أَنفُسِكُمْ تَحِيَّةً
مِّنْ عِندِ اللهِ مُبَارَكَةً طَيِّبَةً ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللهُ لَكُمُ
الْآيَاتِ لَعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ
Laysa AAala al-aAAma harajunwala AAala al-aAAraji harajun walaAAala almareedi
harajun wala AAalaanfusikum an ta/kuloo min buyootikum aw buyooti aba-ikumaw
buyooti ommahatikum aw buyooti ikhwanikum awbuyooti akhawatikum aw buyooti
aAAmamikum awbuyooti AAammatikum aw buyooti akhwalikum awbuyooti khalatikum aw
ma malaktum mafatihahuaw sadeeqikum laysa AAalaykum junahun an ta/kuloojameeAAan
aw ashtatan fa-itha dakhaltum buyootanfasallimoo AAala anfusikum tahiyyatan min
AAindiAllahi mubarakatan tayyibatan kathalikayubayyinu Allahu lakumu al-ayati
laAAallakumtaAAqiloon
Swahili
Si vibaya kwa kipofu, wala si vibaya kwa kiguru, wala si vibaya kwa mgonjwa,
wala kwenu nyinyi, mkila katika nyumba zenu, au nyumba za baba zenu, au nyumba
za mama zenu, au nyumba za kaka zenu, au nyumba za dada zenu, au nyumba za ami
zenu, au nyumba za shangazi zenu, au nyumba za wajomba zenu, au nyumba za dada
wa mama zenu, au za mlio washikia funguo zao, au rafiki yenu. Si vibaya kwenu
mkila pamoja au mbali mbali. Na mkiingia katika nyumba, toleaneni salamu, kuwa
ni maamkio yanayo toka kwa Mwenyezi Mungu, yenye baraka na mema. Hivyo ndivyo
Mwenyezi Mungu anavyo kubainishieni Aya zake mpate kuelewa.
|
Ayah 24:62 الأية
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ آمَنُوا بِاللهِ وَرَسُولِهِ وَإِذَا كَانُوا
مَعَهُ عَلَىٰ أَمْرٍ جَامِعٍ لَّمْ يَذْهَبُوا حَتَّىٰ يَسْتَأْذِنُوهُ ۚ إِنَّ
الَّذِينَ يَسْتَأْذِنُونَكَ أُولَٰئِكَ الَّذِينَ يُؤْمِنُونَ بِاللهِ
وَرَسُولِهِ ۚ فَإِذَا اسْتَأْذَنُوكَ لِبَعْضِ شَأْنِهِمْ فَأْذَن لِّمَن شِئْتَ
مِنْهُمْ وَاسْتَغْفِرْ لَهُمُ اللهَ ۚ إِنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ
Innama almu/minoona allatheenaamanoo billahi warasoolihi wa-itha kanoomaAAahu
AAala amrin jamiAAin lam yathhaboo hattayasta/thinoohu inna allatheena
yasta/thinoonakaola-ika allatheena yu/minoona billahiwarasoolihi fa-itha
ista/thanooka libaAAdisha/nihim fa/than liman shi/ta minhum wastaghfirlahumu
Allaha inna Allaha ghafoorun raheem
Swahili
Hakika Waumini wa kweli ni walio muamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake; na wanapo
kuwa pamoja naye kwa jambo la kuwakhusu wote hawaondoki mpaka wamtake ruhusa.
Kwa hakika wale wanao kuomba ruhusa, hao ndio wanao muamini Mwenyezi Mungu na
Mtume wake. Na wakikuomba ruhusa kwa baadhi ya kazi zao, mruhusu umtakaye
miongoni mwao, uwaombee msamaha kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni
Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemmu.
|
Ayah 24:63 الأية
لَّا تَجْعَلُوا دُعَاءَ الرَّسُولِ بَيْنَكُمْ كَدُعَاءِ بَعْضِكُم بَعْضًا ۚ قَدْ
يَعْلَمُ اللهُ الَّذِينَ يَتَسَلَّلُونَ مِنكُمْ لِوَاذًا ۚ فَلْيَحْذَرِ
الَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنْ أَمْرِهِ أَن تُصِيبَهُمْ فِتْنَةٌ أَوْ يُصِيبَهُمْ
عَذَابٌ أَلِيمٌ
La tajAAaloo duAAaa arrasoolibaynakum kaduAAa-i baAAdikum baAAdan qadyaAAlamu
Allahu allatheena yatasallaloona minkumliwathan falyahthari allatheena
yukhalifoonaAAan amrihi an tuseebahum fitnatun aw yuseebahumAAathabun aleem
Swahili
Msifanye wito wa Mtume baina yenu kama wito wa nyinyi kwa nyinyi. Hakika
Mwenyezi Mungu anawajua miongoni mwenu wanao ondoka kwa uficho. Basi
nawatahadhari wanao khalifu amri yake, usije ukawapata msiba au ikawapata adhabu
chungu.
|
Ayah 24:64 الأية
أَلَا إِنَّ لِلَّهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ قَدْ يَعْلَمُ مَا
أَنتُمْ عَلَيْهِ وَيَوْمَ يُرْجَعُونَ إِلَيْهِ فَيُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُوا ۗ
وَاللهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
Ala inna lillahi ma feeassamawati wal-ardi qadyaAAlamu ma antum AAalayhi wayawma
yurjaAAoona ilayhifayunabbi-ohum bima AAamiloo wallahubikulli shay-in AAaleem
Swahili
Jueni kuwa hakika ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na ardhini. Hakika
Yeye anajua mlio nayo. Na siku mtapo rudishwa kwake atawaeleza waliyo yafanya.
Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.
|
©
EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us
|