1st Ayah 1 الأية ١الأوليبِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ
وَالصَّافَّاتِ صَفًّا
Wassaffati saffa
Swahili
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
|
Ayah 37:2 الأية
فَالزَّاجِرَاتِ زَجْرًا
Fazzajirati zajra
Swahili
Na kwa wenye kukataza mabaya.
|
Ayah 37:3 الأية
فَالتَّالِيَاتِ ذِكْرًا
Fattaliyati thikra
Swahili
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
|
Ayah 37:4 الأية
إِنَّ إِلَٰهَكُمْ لَوَاحِدٌ
Inna ilahakum lawahid
Swahili
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
|
Ayah 37:5 الأية
رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ
Rabbu assamawati wal-ardiwama baynahuma warabbu almashariq
Swahili
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa
mashariki zote.
|
Ayah 37:6 الأية
إِنَّا زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِزِينَةٍ الْكَوَاكِبِ
Inna zayyanna assamaaaddunya bizeenatin alkawakib
Swahili
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
|
Ayah 37:7 الأية
وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَانٍ مَّارِدٍ
Wahifthan min kulli shaytaninmarid
Swahili
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
|
Ayah 37:8 الأية
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى الْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ
La yassammaAAoona ila almala-ial-aAAla wayuqthafoona min kulli janib
Swahili
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
|
Ayah 37:9 الأية
دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ
Duhooran walahum AAathabun wasib
Swahili
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
|
Ayah 37:10 الأية
إِلَّا مَنْ خَطِفَ الْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ ثَاقِبٌ
Illa man khatifa alkhatfatafaatbaAAahu shihabun thaqib
Swahili
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
|
Ayah 37:11 الأية
فَاسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَا ۚ إِنَّا خَلَقْنَاهُم
مِّن طِينٍ لَّازِبٍ
Fastaftihim ahum ashaddu khalqan amman khalaqna inna khalaqnahum min teeninlazib
Swahili
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba.
Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
|
Ayah 37:12 الأية
بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ
Bal AAajibta wayaskharoon
Swahili
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
|
Ayah 37:13 الأية
وَإِذَا ذُكِّرُوا لَا يَذْكُرُونَ
Wa-itha thukkiroo la yathkuroon
Swahili
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
|
Ayah 37:14 الأية
وَإِذَا رَأَوْا آيَةً يَسْتَسْخِرُونَ
Wa-itha raaw ayatanyastaskhiroon
Swahili
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
|
Ayah 37:15 الأية
وَقَالُوا إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ
Waqaloo in hatha illasihrun mubeen
Swahili
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
|
Ayah 37:16 الأية
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
A-itha mitna wakunnaturaban waAAithaman a-innalamabAAoothoon
Swahili
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
|
Ayah 37:17 الأية
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ
Awa abaona al-awwaloon
Swahili
Hata baba zetu wa zamani?
|
Ayah 37:18 الأية
قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَاخِرُونَ
Qul naAAam waantum dakhiroon
Swahili
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
|
Ayah 37:19 الأية
فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ
Fa-innama hiya zajratun wahidatunfa-itha hum yanthuroon
Swahili
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
|
Ayah 37:20 الأية
وَقَالُوا يَا وَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ الدِّينِ
Waqaloo ya waylana hathayawmu addeen
Swahili
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
|
Ayah 37:21 الأية
هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ
Hatha yawmu alfasli allatheekuntum bihi tukaththiboon
Swahili
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
|
Ayah 37:22 الأية
احْشُرُوا الَّذِينَ ظَلَمُوا وَأَزْوَاجَهُمْ وَمَا كَانُوا يَعْبُدُونَ
Ohshuroo allatheena thalamoowaazwajahum wama kanoo yaAAbudoon
Swahili
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
|
Ayah 37:23 الأية
مِن دُونِ اللهِ فَاهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْجَحِيمِ
Min dooni Allahi fahdoohum ilasirati aljaheem
Swahili
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
|
Ayah 37:24 الأية
وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْئُولُونَ
Waqifoohum innahum masooloon
Swahili
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
|
Ayah 37:25 الأية
مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ
Ma lakum la tanasaroon
Swahili
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
|
Ayah 37:26 الأية
بَلْ هُمُ الْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ
Bal humu alyawma mustaslimoon
Swahili
Bali hii leo, watasalimu amri.
|
Ayah 37:27 الأية
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ
Waaqbala baAAduhum AAala baAAdinyatasaaloon
Swahili
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
|
Ayah 37:28 الأية
قَالُوا إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ الْيَمِينِ
Qaloo innakum kuntum ta/toonanaAAani alyameen
Swahili
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
|
Ayah 37:29 الأية
قَالُوا بَل لَّمْ تَكُونُوا مُؤْمِنِينَ
Qaloo bal lam takoonoo mu/mineen
Swahili
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
|
Ayah 37:30 الأية
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَاغِينَ
Wama kana lanaAAalaykum min sultanin bal kuntum qawman tagheen
Swahili
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
|
Ayah 37:31 الأية
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَا ۖ إِنَّا لَذَائِقُونَ
Fahaqqa AAalayna qawlu rabbinainna latha-iqoon
Swahili
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka
tutaonja tu adhabu.
|
Ayah 37:32 الأية
فَأَغْوَيْنَاكُمْ إِنَّا كُنَّا غَاوِينَ
Faaghwaynakum inna kunnaghaween
Swahili
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
|
Ayah 37:33 الأية
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ
Fa-innahum yawma-ithin fee alAAathabimushtarikoon
Swahili
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
|
Ayah 37:34 الأية
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ
Inna kathalika nafAAalu bilmujrimeen
Swahili
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
|
Ayah 37:35 الأية
إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَٰهَ إِلَّا اللهُ يَسْتَكْبِرُونَ
Innahum kanoo itha qeela lahumla ilaha illa Allahu yastakbiroon
Swahili
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu
tu, wakijivuna.
|
Ayah 37:36 الأية
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ
Wayaqooloona a-inna latarikoo alihatinalishaAAirin majnoon
Swahili
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi
mwendawazimu?
|
Ayah 37:37 الأية
بَلْ جَاءَ بِالْحَقِّ وَصَدَّقَ الْمُرْسَلِينَ
Bal jaa bilhaqqi wasaddaqaalmursaleen
Swahili
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
|
Ayah 37:38 الأية
إِنَّكُمْ لَذَائِقُو الْعَذَابِ الْأَلِيمِ
Innakum latha-iqoo alAAathabial-aleem
Swahili
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
|
Ayah 37:39 الأية
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Wama tujzawna illa makuntum taAAmaloon
Swahili
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
|
Ayah 37:40 الأية
إِلَّا عِبَادَ اللهِ الْمُخْلَصِينَ
Illa AAibada Allahialmukhlaseen
Swahili
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
|
Ayah 37:41 الأية
أُولَٰئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ
Ola-ika lahum rizqun maAAloom
Swahili
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
|
Ayah 37:42 الأية
فَوَاكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ
Fawakihu wahum mukramoon
Swahili
Matunda, nao watahishimiwa.
|
Ayah 37:43 الأية
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ
Fee jannati annaAAeem
Swahili
Katika Bustani za neema.
|
Ayah 37:44 الأية
عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَابِلِينَ
AAala sururin mutaqabileen
Swahili
Wako juu ya viti wamekabiliana.
|
Ayah 37:45 الأية
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ
Yutafu AAalayhim bika/sin min maAAeen
Swahili
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
|
Ayah 37:46 الأية
بَيْضَاءَ لَذَّةٍ لِّلشَّارِبِينَ
Baydaa laththatin lishsharibeen
Swahili
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
|
Ayah 37:47 الأية
لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ
La feeha ghawlun walahum AAanha yunzafoon
Swahili
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
|
Ayah 37:48 الأية
وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ عِينٌ
WaAAindahum qasiratu attarfiAAeen
Swahili
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
|
Ayah 37:49 الأية
كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ
Kaannahunna baydun maknoon
Swahili
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
|
Ayah 37:50 الأية
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ
Faaqbala baAAduhum AAala baAAdinyatasaaloon
Swahili
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
|
Ayah 37:51 الأية
قَالَ قَائِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٌ
Qala qa-ilun minhum innee kanalee qareen
Swahili
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
|
Ayah 37:52 الأية
يَقُولُ أَإِنَّكَ لَمِنَ الْمُصَدِّقِينَ
Yaqoolu a-innaka lamina almusaddiqeen
Swahili
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
|
Ayah 37:53 الأية
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَدِينُونَ
A-itha mitna wakunnaturaban waAAithaman a-innalamadeenoon
Swahili
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
|
Ayah 37:54 الأية
قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Qala hal antum muttaliAAoon
Swahili
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
|
Ayah 37:55 الأية
فَاطَّلَعَ فَرَآهُ فِي سَوَاءِ الْجَحِيمِ
FattalaAAa faraahu feesawa-i aljaheem
Swahili
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
|
Ayah 37:56 الأية
قَالَ تَاللهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ
Qala tallahi in kidtalaturdeen
Swahili
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
|
Ayah 37:57 الأية
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ الْمُحْضَرِينَ
Walawla niAAmatu rabbee lakuntu minaalmuhdareen
Swahili
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa
walio hudhurishwa.
|
Ayah 37:58 الأية
أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ
Afama nahnu bimayyiteen
Swahili
Je! Sisi hatutakufa,
|
Ayah 37:59 الأية
إِلَّا مَوْتَتَنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ
Illa mawtatana al-oolawama nahnu bimuAAaththabeen
Swahili
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
|
Ayah 37:60 الأية
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
Inna hatha lahuwa alfawzu alAAatheem
Swahili
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
|
Ayah 37:61 الأية
لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ الْعَامِلُونَ
Limithli hatha falyaAAmali alAAamiloon
Swahili
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
|
Ayah 37:62 الأية
أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ الزَّقُّومِ
Athalika khayrun nuzulan am shajaratuazzaqqoom
Swahili
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
|
Ayah 37:63 الأية
إِنَّا جَعَلْنَاهَا فِتْنَةً لِّلظَّالِمِينَ
Inna jaAAalnahafitnatan liththalimeen
Swahili
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
|
Ayah 37:64 الأية
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِي أَصْلِ الْجَحِيمِ
Innaha shajaratun takhruju fee aslialjaheem
Swahili
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
|
Ayah 37:65 الأية
طَلْعُهَا كَأَنَّهُ رُءُوسُ الشَّيَاطِينِ
TalAAuha kaannahu ruoosu ashshayateen
Swahili
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
|
Ayah 37:66 الأية
فَإِنَّهُمْ لَآكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ
Fa-innahum laakiloona minhafamali-oona minha albutoon
Swahili
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
|
Ayah 37:67 الأية
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ
Thumma inna lahum AAalayha lashawbanmin hameem
Swahili
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
|
Ayah 37:68 الأية
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى الْجَحِيمِ
Thumma inna marjiAAahum la-ila aljaheem
Swahili
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
|
Ayah 37:69 الأية
إِنَّهُمْ أَلْفَوْا آبَاءَهُمْ ضَالِّينَ
Innahum alfaw abaahum dalleen
Swahili
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
|
Ayah 37:70 الأية
فَهُمْ عَلَىٰ آثَارِهِمْ يُهْرَعُونَ
Fahum AAala atharihimyuhraAAoon
Swahili
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
|
Ayah 37:71 الأية
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ الْأَوَّلِينَ
Walaqad dalla qablahum aktharual-awwaleen
Swahili
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
|
Ayah 37:72 الأية
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Walaqad arsalna feehim munthireen
Swahili
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
|
Ayah 37:73 الأية
فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُنذَرِينَ
Fanthur kayfa kanaAAaqibatu almunthareen
Swahili
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
|
Ayah 37:74 الأية
إِلَّا عِبَادَ اللهِ الْمُخْلَصِينَ
Illa AAibada Allahialmukhlaseen
Swahili
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
|
Ayah 37:75 الأية
وَلَقَدْ نَادَانَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ الْمُجِيبُونَ
Walaqad nadana noohunfalaniAAma almujeeboon
Swahili
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
|
Ayah 37:76 الأية
وَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ
Wanajjaynahu waahlahu mina alkarbialAAatheem
Swahili
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
|
Ayah 37:77 الأية
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُ هُمُ الْبَاقِينَ
WajaAAalna thurriyyatahu humualbaqeen
Swahili
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
|
Ayah 37:78 الأية
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ
Watarakna AAalayhi fee al-akhireen
Swahili
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
|
Ayah 37:79 الأية
سَلَامٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِي الْعَالَمِينَ
Salamun AAala noohinfee alAAalameen
Swahili
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
|
Ayah 37:80 الأية
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Inna kathalika najzee almuhsineen
Swahili
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
|
Ayah 37:81 الأية
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ
Innahu min AAibadinaalmu/mineen
Swahili
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
|
Ayah 37:82 الأية
ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ
Thumma aghraqna al-akhareen
Swahili
Kisha tukawazamisha wale wengine.
|
Ayah 37:83 الأية
وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِ لَإِبْرَاهِيمَ
Wa-inna min sheeAAatihi la-ibraheem
Swahili
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
|
Ayah 37:84 الأية
إِذْ جَاءَ رَبَّهُ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Ith jaa rabbahu biqalbinsaleem
Swahili
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
|
Ayah 37:85 الأية
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَاذَا تَعْبُدُونَ
Ith qala li-abeehi waqawmihi mathataAAbudoon
Swahili
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
|
Ayah 37:86 الأية
أَئِفْكًا آلِهَةً دُونَ اللهِ تُرِيدُونَ
A-ifkan alihatan doona Allahitureedoon
Swahili
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
|
Ayah 37:87 الأية
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Fama thannukum birabbialAAalameen
Swahili
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
|
Ayah 37:88 الأية
فَنَظَرَ نَظْرَةً فِي النُّجُومِ
Fanathara nathratanfee annujoom
Swahili
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
|
Ayah 37:89 الأية
فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٌ
Faqala innee saqeem
Swahili
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
|
Ayah 37:90 الأية
فَتَوَلَّوْا عَنْهُ مُدْبِرِينَ
Fatawallaw AAanhu mudbireen
Swahili
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
|
Ayah 37:91 الأية
فَرَاغَ إِلَىٰ آلِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
Faragha ila alihatihimfaqala ala ta/kuloon
Swahili
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
|
Ayah 37:92 الأية
مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ
Ma lakum la tantiqoon
Swahili
Mna nini hata hamsemi?
|
Ayah 37:93 الأية
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًا بِالْيَمِينِ
Faragha AAalayhim darban bilyameen
Swahili
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
|
Ayah 37:94 الأية
فَأَقْبَلُوا إِلَيْهِ يَزِفُّونَ
Faaqbaloo ilayhi yaziffoon
Swahili
Basi wakamjia upesi upesi.
|
Ayah 37:95 الأية
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ
Qala ataAAbudoona ma tanhitoon
Swahili
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
|
Ayah 37:96 الأية
وَاللهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
Wallahu khalaqakum wamataAAmaloon
Swahili
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
|
Ayah 37:97 الأية
قَالُوا ابْنُوا لَهُ بُنْيَانًا فَأَلْقُوهُ فِي الْجَحِيمِ
Qaloo ibnoo lahu bunyananfaalqoohu fee aljaheem
Swahili
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
|
Ayah 37:98 الأية
فَأَرَادُوا بِهِ كَيْدًا فَجَعَلْنَاهُمُ الْأَسْفَلِينَ
Faaradoo bihi kaydan fajaAAalnahumual-asfaleen
Swahili
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
|
Ayah 37:99 الأية
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهْدِينِ
Waqala innee thahibun ilarabbee sayahdeen
Swahili
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
|
Ayah 37:100 الأية
رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ
Rabbi hablee mina assaliheen
Swahili
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
|
Ayah 37:101 الأية
فَبَشَّرْنَاهُ بِغُلَامٍ حَلِيمٍ
Fabashsharnahu bighulamin haleem
Swahili
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
|
Ayah 37:102 الأية
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَا بُنَيَّ إِنِّي أَرَىٰ فِي الْمَنَامِ
أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ
ۖ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللهُ مِنَ الصَّابِرِينَ
Falamma balagha maAAahu assaAAyaqala ya bunayya innee ara fee almanamiannee
athbahuka fanthur mathatara qala ya abati ifAAal ma tu/marusatajidunee in shaa
Allahu mina assabireen
Swahili
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe
mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe,
waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi,
Inshallah, katika wanao subiri.
|
Ayah 37:103 الأية
فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّهُ لِلْجَبِينِ
Falamma aslama watallahuliljabeen
Swahili
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
|
Ayah 37:104 الأية
وَنَادَيْنَاهُ أَن يَا إِبْرَاهِيمُ
Wanadaynahu an ya ibraheem
Swahili
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
|
Ayah 37:105 الأية
قَدْ صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Qad saddaqta arru/yainna kathalika najzee almuhsineen
Swahili
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
|
Ayah 37:106 الأية
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْبَلَاءُ الْمُبِينُ
Inna hatha lahuwa albalaoalmubeen
Swahili
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
|
Ayah 37:107 الأية
وَفَدَيْنَاهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ
Wafadaynahu bithibhinAAatheem
Swahili
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
|
Ayah 37:108 الأية
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ
Watarakna AAalayhi fee al-akhireen
Swahili
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
|
Ayah 37:109 الأية
سَلَامٌ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ
Salamun AAala ibraheem
Swahili
Iwe salama kwa Ibrahim!
|
Ayah 37:110 الأية
كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ
Kathalika najzee almuhsineen
Swahili
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
|
Ayah 37:111 الأية
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ
Innahu min AAibadinaalmu/mineen
Swahili
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
|
Ayah 37:112 الأية
وَبَشَّرْنَاهُ بِإِسْحَاقَ نَبِيًّا مِّنَ الصَّالِحِينَ
Wabashsharnahu bi-ishaqanabiyyan mina assaliheen
Swahili
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
|
Ayah 37:113 الأية
وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰ إِسْحَاقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ
وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ مُبِينٌ
Wabarakna AAalayhi waAAalaishaqa wamin thurriyyatihima muhsinunwathalimun
linafsihi mubeen
Swahili
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na
wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
|
Ayah 37:114 الأية
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ
Walaqad mananna AAala moosawaharoon
Swahili
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
|
Ayah 37:115 الأية
وَنَجَّيْنَاهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ
Wanajjaynahuma waqawmahumamina alkarbi alAAatheem
Swahili
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
|
Ayah 37:116 الأية
وَنَصَرْنَاهُمْ فَكَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ
Wanasarnahum fakanoohumu alghalibeen
Swahili
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
|
Ayah 37:117 الأية
وَآتَيْنَاهُمَا الْكِتَابَ الْمُسْتَبِينَ
Waataynahuma alkitabaalmustabeen
Swahili
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
|
|