Prev  

36. Surah Yâ­Sîn. سورة يس

  Next  



Ayah  36:1  الأية
    +/- -/+  
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Ayah  36:2  الأية
    +/- -/+  

Ayah  36:3  الأية
    +/- -/+  

Ayah  36:4  الأية
    +/- -/+  

Ayah  36:5  الأية
    +/- -/+  

Ayah  36:6  الأية
    +/- -/+  
لِتُنذِرَ قَوْمًا مَّا أُنذِرَ آبَاؤُهُمْ فَهُمْ غَافِلُونَ
Swahili
 
Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa , basi wao wamekuwa wenye kughafilika.

Ayah  36:7  الأية
    +/- -/+  
لَقَدْ حَقَّ الْقَوْلُ عَلَىٰ أَكْثَرِهِمْ فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ
Swahili
 
Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.

Ayah  36:8  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا جَعَلْنَا فِي أَعْنَاقِهِمْ أَغْلَالًا فَهِيَ إِلَى الْأَذْقَانِ فَهُم مُّقْمَحُونَ
Swahili
 
Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.

Ayah  36:9  الأية
    +/- -/+  
وَجَعَلْنَا مِن بَيْنِ أَيْدِيهِمْ سَدًّا وَمِنْ خَلْفِهِمْ سَدًّا فَأَغْشَيْنَاهُمْ فَهُمْ لَا يُبْصِرُونَ
Swahili
 
Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.

Ayah  36:10  الأية
    +/- -/+  
وَسَوَاءٌ عَلَيْهِمْ أَأَنذَرْتَهُمْ أَمْ لَمْ تُنذِرْهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ
Swahili
 
Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.

Ayah  36:11  الأية
    +/- -/+  
إِنَّمَا تُنذِرُ مَنِ اتَّبَعَ الذِّكْرَ وَخَشِيَ الرَّحْمَٰنَ بِالْغَيْبِ ۖ فَبَشِّرْهُ بِمَغْفِرَةٍ وَأَجْرٍ كَرِيمٍ
Swahili
 
Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.

Ayah  36:12  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا نَحْنُ نُحْيِي الْمَوْتَىٰ وَنَكْتُبُ مَا قَدَّمُوا وَآثَارَهُمْ ۚ وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ فِي إِمَامٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.

Ayah  36:13  الأية
    +/- -/+  
وَاضْرِبْ لَهُم مَّثَلًا أَصْحَابَ الْقَرْيَةِ إِذْ جَاءَهَا الْمُرْسَلُونَ
Swahili
 
Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.

Ayah  36:14  الأية
    +/- -/+  
إِذْ أَرْسَلْنَا إِلَيْهِمُ اثْنَيْنِ فَكَذَّبُوهُمَا فَعَزَّزْنَا بِثَالِثٍ فَقَالُوا إِنَّا إِلَيْكُم مُّرْسَلُونَ
Swahili
 
Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.

Ayah  36:15  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا مَا أَنتُمْ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَمَا أَنزَلَ الرَّحْمَٰنُ مِن شَيْءٍ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا تَكْذِبُونَ
Swahili
 
Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.

Ayah  36:16  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا رَبُّنَا يَعْلَمُ إِنَّا إِلَيْكُمْ لَمُرْسَلُونَ
Swahili
 
Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.

Ayah  36:17  الأية
    +/- -/+  
وَمَا عَلَيْنَا إِلَّا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ
Swahili
 
Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.

Ayah  36:18  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا إِنَّا تَطَيَّرْنَا بِكُمْ ۖ لَئِن لَّمْ تَنتَهُوا لَنَرْجُمَنَّكُمْ وَلَيَمَسَّنَّكُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٌ
Swahili
 
Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.

Ayah  36:19  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا طَائِرُكُم مَّعَكُمْ ۚ أَئِن ذُكِّرْتُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ مُّسْرِفُونَ
Swahili
 
Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.

Ayah  36:20  الأية
    +/- -/+  
وَجَاءَ مِنْ أَقْصَى الْمَدِينَةِ رَجُلٌ يَسْعَىٰ قَالَ يَا قَوْمِ اتَّبِعُوا الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.

Ayah  36:21  الأية
    +/- -/+  
اتَّبِعُوا مَن لَّا يَسْأَلُكُمْ أَجْرًا وَهُم مُّهْتَدُونَ
Swahili
 
Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.

Ayah  36:22  الأية
    +/- -/+  
وَمَا لِيَ لَا أَعْبُدُ الَّذِي فَطَرَنِي وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ
Swahili
 
NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?

Ayah  36:23  الأية
    +/- -/+  
أَأَتَّخِذُ مِن دُونِهِ آلِهَةً إِن يُرِدْنِ الرَّحْمَٰنُ بِضُرٍّ لَّا تُغْنِ عَنِّي شَفَاعَتُهُمْ شَيْئًا وَلَا يُنقِذُونِ
Swahili
 
Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.

Ayah  36:24  الأية
    +/- -/+  
إِنِّي إِذًا لَّفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.

Ayah  36:25  الأية
    +/- -/+  
إِنِّي آمَنتُ بِرَبِّكُمْ فَاسْمَعُونِ
Swahili
 
Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!

Ayah  36:26  الأية
    +/- -/+  
قِيلَ ادْخُلِ الْجَنَّةَ ۖ قَالَ يَا لَيْتَ قَوْمِي يَعْلَمُونَ
Swahili
 
Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua

Ayah  36:27  الأية
    +/- -/+  
بِمَا غَفَرَ لِي رَبِّي وَجَعَلَنِي مِنَ الْمُكْرَمِينَ
Swahili
 
Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa.

Ayah  36:28  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَنزَلْنَا عَلَىٰ قَوْمِهِ مِن بَعْدِهِ مِن جُندٍ مِّنَ السَّمَاءِ وَمَا كُنَّا مُنزِلِينَ
Swahili
 
Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.

Ayah  36:29  الأية
    +/- -/+  
إِن كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ خَامِدُونَ
Swahili
 
Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!

Ayah  36:30  الأية
    +/- -/+  
يَا حَسْرَةً عَلَى الْعِبَادِ ۚ مَا يَأْتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
Swahili
 
Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.

Ayah  36:31  الأية
    +/- -/+  
أَلَمْ يَرَوْا كَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّنَ الْقُرُونِ أَنَّهُمْ إِلَيْهِمْ لَا يَرْجِعُونَ
Swahili
 
Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.

Ayah  36:32  الأية
    +/- -/+  
وَإِن كُلٌّ لَّمَّا جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ
Swahili
 
Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.

Ayah  36:33  الأية
    +/- -/+  
وَآيَةٌ لَّهُمُ الْأَرْضُ الْمَيْتَةُ أَحْيَيْنَاهَا وَأَخْرَجْنَا مِنْهَا حَبًّا فَمِنْهُ يَأْكُلُونَ
Swahili
 
Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila!

Ayah  36:34  الأية
    +/- -/+  
وَجَعَلْنَا فِيهَا جَنَّاتٍ مِّن نَّخِيلٍ وَأَعْنَابٍ وَفَجَّرْنَا فِيهَا مِنَ الْعُيُونِ
Swahili
 
Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake,

Ayah  36:35  الأية
    +/- -/+  
لِيَأْكُلُوا مِن ثَمَرِهِ وَمَا عَمِلَتْهُ أَيْدِيهِمْ ۖ أَفَلَا يَشْكُرُونَ
Swahili
 
Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?

Ayah  36:36  الأية
    +/- -/+  
سُبْحَانَ الَّذِي خَلَقَ الْأَزْوَاجَ كُلَّهَا مِمَّا تُنبِتُ الْأَرْضُ وَمِنْ أَنفُسِهِمْ وَمِمَّا لَا يَعْلَمُونَ
Swahili
 
Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.

Ayah  36:37  الأية
    +/- -/+  
وَآيَةٌ لَّهُمُ اللَّيْلُ نَسْلَخُ مِنْهُ النَّهَارَ فَإِذَا هُم مُّظْلِمُونَ
Swahili
 
Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.

Ayah  36:38  الأية
    +/- -/+  
وَالشَّمْسُ تَجْرِي لِمُسْتَقَرٍّ لَّهَا ۚ ذَٰلِكَ تَقْدِيرُ الْعَزِيزِ الْعَلِيمِ
Swahili
 
Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.

Ayah  36:39  الأية
    +/- -/+  
وَالْقَمَرَ قَدَّرْنَاهُ مَنَازِلَ حَتَّىٰ عَادَ كَالْعُرْجُونِ الْقَدِيمِ
Swahili
 
Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.

Ayah  36:40  الأية
    +/- -/+  
لَا الشَّمْسُ يَنبَغِي لَهَا أَن تُدْرِكَ الْقَمَرَ وَلَا اللَّيْلُ سَابِقُ النَّهَارِ ۚ وَكُلٌّ فِي فَلَكٍ يَسْبَحُونَ
Swahili
 
Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.

Ayah  36:41  الأية
    +/- -/+  
وَآيَةٌ لَّهُمْ أَنَّا حَمَلْنَا ذُرِّيَّتَهُمْ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ
Swahili
 
Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.

Ayah  36:42  الأية
    +/- -/+  
وَخَلَقْنَا لَهُم مِّن مِّثْلِهِ مَا يَرْكَبُونَ
Swahili
 
Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.

Ayah  36:43  الأية
    +/- -/+  
وَإِن نَّشَأْ نُغْرِقْهُمْ فَلَا صَرِيخَ لَهُمْ وَلَا هُمْ يُنقَذُونَ
Swahili
 
Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,

Ayah  36:44  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا رَحْمَةً مِّنَّا وَمَتَاعًا إِلَىٰ حِينٍ
Swahili
 
Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.

Ayah  36:45  الأية
    +/- -/+  
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ اتَّقُوا مَا بَيْنَ أَيْدِيكُمْ وَمَا خَلْفَكُمْ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ
Swahili
 
Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa...

Ayah  36:46  الأية
    +/- -/+  
وَمَا تَأْتِيهِم مِّنْ آيَةٍ مِّنْ آيَاتِ رَبِّهِمْ إِلَّا كَانُوا عَنْهَا مُعْرِضِينَ
Swahili
 
Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye kuipuuza.

Ayah  36:47  الأية
    +/- -/+  
وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ أَنفِقُوا مِمَّا رَزَقَكُمُ اللهُ قَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا أَنُطْعِمُ مَن لَّوْ يَشَاءُ اللهُ أَطْعَمَهُ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.

Ayah  36:48  الأية
    +/- -/+  
وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Swahili
 
Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?

Ayah  36:49  الأية
    +/- -/+  
مَا يَنظُرُونَ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً تَأْخُذُهُمْ وَهُمْ يَخِصِّمُونَ
Swahili
 
Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.

Ayah  36:50  الأية
    +/- -/+  
فَلَا يَسْتَطِيعُونَ تَوْصِيَةً وَلَا إِلَىٰ أَهْلِهِمْ يَرْجِعُونَ
Swahili
 
Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.

Ayah  36:51  الأية
    +/- -/+  
وَنُفِخَ فِي الصُّورِ فَإِذَا هُم مِّنَ الْأَجْدَاثِ إِلَىٰ رَبِّهِمْ يَنسِلُونَ
Swahili
 
Na litapulizwa barugumu, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao Mlezi.

Ayah  36:52  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا يَا وَيْلَنَا مَن بَعَثَنَا مِن مَّرْقَدِنَا ۜ ۗ هَٰذَا مَا وَعَدَ الرَّحْمَٰنُ وَصَدَقَ الْمُرْسَلُونَ
Swahili
 
Watasema: Ole wetu! Nani aliye tufufua kwenye malazi yetu? Haya ndiyo aliyo yaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.

Ayah  36:53  الأية
    +/- -/+  
إِن كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ
Swahili
 
Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu.

Ayah  36:54  الأية
    +/- -/+  
فَالْيَوْمَ لَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَلَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ
Swahili
 
Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyo kuwa mkiyatenda.

Ayah  36:55  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ أَصْحَابَ الْجَنَّةِ الْيَوْمَ فِي شُغُلٍ فَاكِهُونَ
Swahili
 
Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi.

Ayah  36:56  الأية
    +/- -/+  
هُمْ وَأَزْوَاجُهُمْ فِي ظِلَالٍ عَلَى الْأَرَائِكِ مُتَّكِئُونَ
Swahili
 
Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fakhari.

Ayah  36:57  الأية
    +/- -/+  
لَهُمْ فِيهَا فَاكِهَةٌ وَلَهُم مَّا يَدَّعُونَ
Swahili
 
Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakacho kitaka.

Ayah  36:58  الأية
    +/- -/+  
سَلَامٌ قَوْلًا مِّن رَّبٍّ رَّحِيمٍ
Swahili
 
"Salama!" Hiyo ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mlezi Mwenye kurehemu.

Ayah  36:59  الأية
    +/- -/+  
وَامْتَازُوا الْيَوْمَ أَيُّهَا الْمُجْرِمُونَ
Swahili
 
Na enyi wakosefu! Jitengeni leo!

Ayah  36:60  الأية
    +/- -/+  
أَلَمْ أَعْهَدْ إِلَيْكُمْ يَا بَنِي آدَمَ أَن لَّا تَعْبُدُوا الشَّيْطَانَ ۖ إِنَّهُ لَكُمْ عَدُوٌّ مُّبِينٌ
Swahili
 
Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet'ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu.

Ayah  36:61  الأية
    +/- -/+  
وَأَنِ اعْبُدُونِي ۚ هَٰذَا صِرَاطٌ مُّسْتَقِيمٌ
Swahili
 
Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.

Ayah  36:62  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ أَضَلَّ مِنكُمْ جِبِلًّا كَثِيرًا ۖ أَفَلَمْ تَكُونُوا تَعْقِلُونَ
Swahili
 
Na bila ya shaka yeye amekwisha lipoteza kundi kubwa miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkifikiri?

Ayah  36:63  الأية
    +/- -/+  
هَٰذِهِ جَهَنَّمُ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ
Swahili
 
Hii basi ndiyo Jahannamu mliyo kuwa mkiahidiwa.

Ayah  36:64  الأية
    +/- -/+  
اصْلَوْهَا الْيَوْمَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ
Swahili
 
Ingieni leo kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru.

Ayah  36:65  الأية
    +/- -/+  
الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَىٰ أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ
Swahili
 
Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma.

Ayah  36:66  الأية
    +/- -/+  
وَلَوْ نَشَاءُ لَطَمَسْنَا عَلَىٰ أَعْيُنِهِمْ فَاسْتَبَقُوا الصِّرَاطَ فَأَنَّىٰ يُبْصِرُونَ
Swahili
 
Na tungeli penda tungeli yafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wange ionaje?

Ayah  36:67  الأية
    +/- -/+  
وَلَوْ نَشَاءُ لَمَسَخْنَاهُمْ عَلَىٰ مَكَانَتِهِمْ فَمَا اسْتَطَاعُوا مُضِيًّا وَلَا يَرْجِعُونَ
Swahili
 
Na tungeli taka tunge wageuza sura hapo hapo walipo, basi wasinge weza kwenda wala kurudi.

Ayah  36:68  الأية
    +/- -/+  
وَمَن نُّعَمِّرْهُ نُنَكِّسْهُ فِي الْخَلْقِ ۖ أَفَلَا يَعْقِلُونَ
Swahili
 
Na tunaye mzeesha tunamrudisha nyuma katika umbo. Basi je! hawazingatii?

Ayah  36:69  الأية
    +/- -/+  
وَمَا عَلَّمْنَاهُ الشِّعْرَ وَمَا يَنبَغِي لَهُ ۚ إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ وَقُرْآنٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Wala hatukumfundisha (Muhammad) mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur'ani inayo bainisha.

Ayah  36:70  الأية
    +/- -/+  
لِّيُنذِرَ مَن كَانَ حَيًّا وَيَحِقَّ الْقَوْلُ عَلَى الْكَافِرِينَ
Swahili
 
Ili imwonye aliye hai, na neno litimie juu ya makafiri.

Ayah  36:71  الأية
    +/- -/+  
أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّا خَلَقْنَا لَهُم مِّمَّا عَمِلَتْ أَيْدِينَا أَنْعَامًا فَهُمْ لَهَا مَالِكُونَ
Swahili
 
Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyo fanya mikono yetu wanyama wa mifugo, na wao wakawa wenye kuwamiliki.

Ayah  36:72  الأية
    +/- -/+  
وَذَلَّلْنَاهَا لَهُمْ فَمِنْهَا رَكُوبُهُمْ وَمِنْهَا يَأْكُلُونَ
Swahili
 
Na Sisi tukawadhalilishia. Basi baadhi yao wako wanao wapanda, na baadhi yao wanawala.

Ayah  36:73  الأية
    +/- -/+  
وَلَهُمْ فِيهَا مَنَافِعُ وَمَشَارِبُ ۖ أَفَلَا يَشْكُرُونَ
Swahili
 
Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?

Ayah  36:74  الأية
    +/- -/+  
وَاتَّخَذُوا مِن دُونِ اللهِ آلِهَةً لَّعَلَّهُمْ يُنصَرُونَ
Swahili
 
Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu ili ati wapate kusaidiwa!

Ayah  36:75  الأية
    +/- -/+  
لَا يَسْتَطِيعُونَ نَصْرَهُمْ وَهُمْ لَهُمْ جُندٌ مُّحْضَرُونَ
Swahili
 
Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio watakuwa askari wao watakao hudhurishwa.

Ayah  36:76  الأية
    +/- -/+  
فَلَا يَحْزُنكَ قَوْلُهُمْ ۘ إِنَّا نَعْلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعْلِنُونَ
Swahili
 
Basi maneno yao yasikuhuzunishe. Hakika Sisi tunayajua wanayo yaweka siri na wanayo yatangaza.

Ayah  36:77  الأية
    +/- -/+  
أَوَلَمْ يَرَ الْإِنسَانُ أَنَّا خَلَقْنَاهُ مِن نُّطْفَةٍ فَإِذَا هُوَ خَصِيمٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Kwani mwanaadamu haoni ya kwamba Sisi tumemuumba yeye kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndio amekuwa ndiye mgomvi wa dhaahiri!

Ayah  36:78  الأية
    +/- -/+  
وَضَرَبَ لَنَا مَثَلًا وَنَسِيَ خَلْقَهُ ۖ قَالَ مَن يُحْيِي الْعِظَامَ وَهِيَ رَمِيمٌ
Swahili
 
Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: Ni nani huyo atakaye ihuisha mifupa nayo imekwisha mung'unyika?

Ayah  36:79  الأية
    +/- -/+  
قُلْ يُحْيِيهَا الَّذِي أَنشَأَهَا أَوَّلَ مَرَّةٍ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ خَلْقٍ عَلِيمٌ
Swahili
 
Sema: Ataihuisha huyo huyo aliye iumba hapo mara ya mwanzo. Na Yeye ni Mjuzi wa kila kuumba.

Ayah  36:80  الأية
    +/- -/+  
الَّذِي جَعَلَ لَكُم مِّنَ الشَّجَرِ الْأَخْضَرِ نَارًا فَإِذَا أَنتُم مِّنْهُ تُوقِدُونَ
Swahili
 
Aliye kujaalieni kupata moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa kwa huo mnawasha.

Ayah  36:81  الأية
    +/- -/+  
أَوَلَيْسَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يَخْلُقَ مِثْلَهُم ۚ بَلَىٰ وَهُوَ الْخَلَّاقُ الْعَلِيمُ
Swahili
 
Kwani aliye ziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwani! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.

Ayah  36:82  الأية
    +/- -/+  
إِنَّمَا أَمْرُهُ إِذَا أَرَادَ شَيْئًا أَن يَقُولَ لَهُ كُن فَيَكُونُ
Swahili
 
Hakika amri yake anapo taka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kikawa.

Ayah  36:83  الأية
    +/- -/+  
فَسُبْحَانَ الَّذِي بِيَدِهِ مَلَكُوتُ كُلِّ شَيْءٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ
Swahili
 
Basi Ametakasika yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake Yeye mtarejeshwa.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us