Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na makundi mengine baada yao. Na kila
taifa lilikuwa na hamu juu ya Mtume wao wamkamate. Na walibishana kwa upotovu
ili kuipindua haki. Kwa hivyo niliwakamata. Basi ilikuwaje adhabu yangu!
Wale wanao beba A'rshi, na wanao izunguka, wanamsabihi na kumhimidi Mola wao
Mlezi, na wanamuamini, na wanawaombea msamaha walio amini kwa kusema: Mola wetu
Mlezi! Umekienea kila kitu kwa rehema na ujuzi. Basi wasamehe walio tubu na
wakaifuata Njia yako, na waepushe na adhabu ya Jahannamu.
Mola wetu Mlezi! Na waingize katika Bustani za Milele ulizo waahidi. Na uwape
haya pia wale walio fanya mema miongoni mwa wazee wao na wake zao na dhuriya
zao. Hakika Wewe ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
Kwa hakika wale walio kufuru watanadiwa: Bila ya shaka kukuchukieni Mwenyezi
Mungu ni kukubwa kuliko kujichukia nyinyi nafsi zenu, mlipo kuwa mnaitwa kwenye
Imani nanyi mkakataa.
Hayo ni hivyo kwa sababu mlikuwa akiombwa Mwenyezi Mungu peke yake mnakataa. Na
akishirikishwa mnaamini. Basi hukumu ni ya Mwenyezi Mungu Mtukufu Mkuu.
Kwani hawatembei katika ardhi wakaona jinsi ulivyo kuwa mwisho wa walio kuwa
kabla yao? Hao walikuwa wamewazidi hawa kwa nguvu na athari katika nchi. Na
Mwenyezi Mungu aliwatia mkononi kwa sababu ya madhambi yao. Na wala hapakuwa wa
kuwalinda na Mwenyezi Mungu.
Hayo ni kwa sababu walikuwa wanawajia Mitume wao kwa hoja zilizo wazi, lakini
wakawakataa, ndipo Mwenyezi Mungu akawakamata. Bila ya shaka Yeye ni Mwenye
nguvu, Mkali wa kuadhibu.
Basi alipo waletea Haki inayo toka kwetu, walisema: Waueni watoto wanaume wa
wale walio muamini na wawacheni hai wanawake wao. Na haviwi vitimbi vya makafiri
ila katika upotovu.
Na Firauni akasema: Niachieni nimuuwe Musa, naye amwite Mola wake Mlezi! Mimi
nachelea asije kubadilishieni dini yenu, au akatangaza uharibifu katika nchi.
Na akasema mtu mmoja Muumini, aliye kuwa mmoja katika watu wa Firauni aliye
ficha Imani yake: Mtamuuwa mtu kwa sababu anasema Mola wangu Mlezi ni Mwenyezi
Mungu? Na hali naye amekujieni na hoja zilizo wazi? Na akiwa yeye mwongo basi
uwongo wake ni juu yake mwenyewe, na akiwa mkweli yatakufikieni baadhi ya hayo
anayo kuahidini. Hakika Mwenyezi Mungu hamwongoi apindukiaye mipaka, mwongo
mkubwa.
Enyi watu wangu! Leo mna ufalme, mmeshinda katika nchi; basi ni nani atakaye
nisaidia kutuokoa na adhabu ya Mwenyezi Mungu kama ikitufikia? Firauni akasema:
Sikupeni shauri ila ile niliyo iona, wala sikuongozeni ila kwenye njia ya
uwongofu.
Siku mtakapo geuka kurudi nyuma. Hamtakuwa na wa kukulindeni kwa Mwenyezi Mungu.
Na mwenye kuhukumiwa na Mwenyezi Mungu kupotea, basi huyo hana wa kumwongoa.
Na alikwisha wajieni Yusuf zamani kwa dalili zilizo wazi, lakini nyinyi
mliendelea katika shaka kwa yale aliyo kuleteeni; mpaka alipo kufa mkasema:
Mwenyezi Mungu hataleta kabisa Mtume baada yake. Kama hivyo Mwenyezi Mungu
humwacha kupotea anaye pindukia mipaka katika maasi anaye jitia shaka.
Hao ambao wanajadiliana katika Ishara za Mwenyezi Mungu pasipo ushahidi wowote
ulio wafikia, ni chukizo kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu na mbele ya walio amini.
Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu apigavyo muhuri juu ya kila moyo wa jeuri anaye
jivuna.
Njia za mbinguni ili nikamwone Mungu wa Musa. Na kwa hakika mimi bila ya shaka
namjua kuwa ni mwongo tu. Na hivi ndivyo Firauni alivyo pambiwa ubaya wa vitendo
vyake, na akazuiliwa Njia. Na vitimbi vya Firauni havikuwa ila katika kuangamia
tu.
Mwenye kutenda uovu hatalipwa ila sawa na huo uwovu wake, na anaye tenda wema,
akiwa mwanamume au mwanamke, naye ni Muumini, basi hao wataingia Peponi,
waruzukiwe humo bila ya hisabu.
Bila ya shaka mnaye niitia kumuabudu hastahiki wito duniani wala Akhera. Na
hakika marejeo yetu ni kwa Mwenyezi Mungu. Na wanao pindukia mipaka ndio watu wa
Motoni!
Nao watasema: Je! Hawakuwa wakikufikieni Mitume wenu kwa hoja zilio wazi?
Watasema: Kwani? Watasema: Basi ombeni! Na maombi ya makafiri hayawi ila ni
kupotea bure.
Hakika hao wanao bishana katika Ishara za Mwenyezi Mungu bila ya uthibitisho
wowote uliyo wajia, hawana vifuani mwao ila kutaka ukubwa tu, na wala huo
hawaufikilii. Basi jikinge kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia,
Mwenye kuona.
Mwenyezi Mungu aliye kufanyieni usiku ili mpate kutulia humo, na mchana wa
kuonea. Hakika Mwenyezi Mungu bila ya shaka ni Mwenye fadhila juu ya watu,
lakini watu wengi hawashukuru.
Ni Mwenyezi Mungu aliye kufanyieni ardhi kuwa ni pahala pa kukaa, na mbingu kuwa
dari. Na akakutieni sura, na akazifanya nzuri sura zenu, na akakuruzukuni vitu
vizuri. Huyo ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu Mlezi. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu
Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Yeye ndiye aliye Hai - hapana mungu isipo kuwa Yeye. Basi muabuduni Yeye
mkimsafishia Dini Yeye. Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa
walimwengu wote.
Sema: Mimi nimekatazwa kuwaabudu hao mnao waomba badala ya Mwenyezi Mungu,
zilipo nijia hoja zilizo dhaahiri kutokana na Mola wangu Mlezi. Na nimeamrishwa
nisilimu kwa Mola wa walimwengu wote.
Yeye ndiye aliye kuumbeni kwa udongo, kisha kwa tone la manii, kisha kwa pande
la damu, kisha akakutoeni katika hali ya mtoto mchanga, kisha mpate kufikilia
utu uzima, kisha mpate kuwa wazee. Na kati yenu wapo wanao kufa kabla, na ili
mfikie muda ulio kwisha wekwa, na ili mpate kufahamu.
Badala ya Mwenyezi Mungu? Watasema: Wametupotea, bali tangu zamani hatukuwa
tukiomba kitu! Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anawaachia makafiri wapotelee mbali.
Basi subiri, hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ya kweli. Na ama tukikuonyesha
baadhi ya yale tuliyo waahidi au tukikufisha, lakini wao watarudishwa kwetu tu.
Na bila ya shaka tuliwatuma Mitume kabla yako. Wengine katika hao tumekusimulia
khabari zao, na wengine hatukukusimulia. Na haiwi Mtume alete Ishara yoyote ila
kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Basi ikija amri ya Mwenyezi Mungu huhukumiwa kwa
Haki, na hapo wapotofu watakhasiri.
Kwani hawatembei katika ardhi wakaona ulikuwaje mwisho wa walio kuwa kabla yao?
Wao walikuwa wengi kuliko hawa, na wamewashinda kwa nguvu na athari katika nchi.
Wala hayakuwafaa hayo waliyo kuwa wakiyachuma.
Lakini imani yao haikuwa yenye kuwafaa kitu wakati ambao wamekwisha iona adhabu
yetu. Huu ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu ulio kuwa kwa waja wake. Na hapo walio
kufuru walikhasiri.