Prev  

38. Surah Sâd. سورة ص

  Next  



Ayah  38:1  الأية
    +/- -/+  
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Ayah  38:2  الأية
    +/- -/+  
بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي عِزَّةٍ وَشِقَاقٍ
Swahili
 
Lakini walio kufuru wamo katika majivuno na upinzani

Ayah  38:3  الأية
    +/- -/+  
كَمْ أَهْلَكْنَا مِن قَبْلِهِم مِّن قَرْنٍ فَنَادَوا وَّلَاتَ حِينَ مَنَاصٍ
Swahili
 
Mataifa mangapi tumeyaangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwisha pita.

Ayah  38:4  الأية
    +/- -/+  
وَعَجِبُوا أَن جَاءَهُم مُّنذِرٌ مِّنْهُمْ ۖ وَقَالَ الْكَافِرُونَ هَٰذَا سَاحِرٌ كَذَّابٌ
Swahili
 
Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anaye tokana nao wenyewe, na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.

Ayah  38:5  الأية
    +/- -/+  
أَجَعَلَ الْآلِهَةَ إِلَٰهًا وَاحِدًا ۖ إِنَّ هَٰذَا لَشَيْءٌ عُجَابٌ
Swahili
 
Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu.

Ayah  38:6  الأية
    +/- -/+  
وَانطَلَقَ الْمَلَأُ مِنْهُمْ أَنِ امْشُوا وَاصْبِرُوا عَلَىٰ آلِهَتِكُمْ ۖ إِنَّ هَٰذَا لَشَيْءٌ يُرَادُ
Swahili
 
Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililo pangwa.

Ayah  38:7  الأية
    +/- -/+  
مَا سَمِعْنَا بِهَٰذَا فِي الْمِلَّةِ الْآخِرَةِ إِنْ هَٰذَا إِلَّا اخْتِلَاقٌ
Swahili
 
Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu.

Ayah  38:8  الأية
    +/- -/+  
أَأُنزِلَ عَلَيْهِ الذِّكْرُ مِن بَيْنِنَا ۚ بَلْ هُمْ فِي شَكٍّ مِّن ذِكْرِي ۖ بَل لَّمَّا يَذُوقُوا عَذَابِ
Swahili
 
Ati yeye tu ndiye aliye teremshiwa mawaidha peke yake katika sisi? Lakini hao wana shaka na mawaidha yangu, bali hawajaionja adhabu yangu.

Ayah  38:9  الأية
    +/- -/+  
أَمْ عِندَهُمْ خَزَائِنُ رَحْمَةِ رَبِّكَ الْعَزِيزِ الْوَهَّابِ
Swahili
 
Au wanazo wao khazina za rehema za Mola wako Mlezi, Mwenye nguvu, Mpaji?

Ayah  38:10  الأية
    +/- -/+  
أَمْ لَهُم مُّلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ فَلْيَرْتَقُوا فِي الْأَسْبَابِ
Swahili
 
Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo kati yao? Basi nawazipande njia za kwendea huko!

Ayah  38:11  الأية
    +/- -/+  
جُندٌ مَّا هُنَالِكَ مَهْزُومٌ مِّنَ الْأَحْزَابِ
Swahili
 
Hao ni askari watao shindwa miongoni mwa makundi yatayo shindwa.

Ayah  38:12  الأية
    +/- -/+  
كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ وَعَادٌ وَفِرْعَوْنُ ذُو الْأَوْتَادِ
Swahili
 
Walikanusha kabla yao kaumu ya Nuhu, na kina A'adi na Firauni mwenye majengo.

Ayah  38:13  الأية
    +/- -/+  
وَثَمُودُ وَقَوْمُ لُوطٍ وَأَصْحَابُ الْأَيْكَةِ ۚ أُولَٰئِكَ الْأَحْزَابُ
Swahili
 
Na Thamud na kaumu Lut'i na watu wa Machakani. Hayo ndiyo makundi.

Ayah  38:14  الأية
    +/- -/+  
إِن كُلٌّ إِلَّا كَذَّبَ الرُّسُلَ فَحَقَّ عِقَابِ
Swahili
 
Hao wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahiki adhabu yangu.

Ayah  38:15  الأية
    +/- -/+  
وَمَا يَنظُرُ هَٰؤُلَاءِ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً مَّا لَهَا مِن فَوَاقٍ
Swahili
 
Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda.

Ayah  38:16  الأية
    +/- -/+  
وَقَالُوا رَبَّنَا عَجِّل لَّنَا قِطَّنَا قَبْلَ يَوْمِ الْحِسَابِ
Swahili
 
Na wao husema: Mola wetu Mlezi! Tuletee upesi sehemu yetu ya adhabu kabla ya Siku ya Hisabu.

Ayah  38:17  الأية
    +/- -/+  
اصْبِرْ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَاذْكُرْ عَبْدَنَا دَاوُودَ ذَا الْأَيْدِ ۖ إِنَّهُ أَوَّابٌ
Swahili
 
Subiri kwa hayo wayasemayo, na umkumbuke mja wetu Daudi, mwenye nguvu. Hakika yeye alikuwa mwingi wa kutubia.

Ayah  38:18  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا سَخَّرْنَا الْجِبَالَ مَعَهُ يُسَبِّحْنَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِشْرَاقِ
Swahili
 
Hakika tuliidhalilisha milima pamoja naye ikisabihi jioni na asubuhi pamoja naye.

Ayah  38:19  الأية
    +/- -/+  
وَالطَّيْرَ مَحْشُورَةً ۖ كُلٌّ لَّهُ أَوَّابٌ
Swahili
 
Na pia ndege walio kusanywa makundi kwa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake.

Ayah  38:20  الأية
    +/- -/+  
وَشَدَدْنَا مُلْكَهُ وَآتَيْنَاهُ الْحِكْمَةَ وَفَصْلَ الْخِطَابِ
Swahili
 
Na tukautia nguvu ufalme wake, na tukampa hikima, na kukata hukumu.

Ayah  38:21  الأية
    +/- -/+  
وَهَلْ أَتَاكَ نَبَأُ الْخَصْمِ إِذْ تَسَوَّرُوا الْمِحْرَابَ
Swahili
 
Na je! Imekufikia khabari ya wagombanao walipo pindukia ukuta kuingia chumbani?

Ayah  38:22  الأية
    +/- -/+  
إِذْ دَخَلُوا عَلَىٰ دَاوُودَ فَفَزِعَ مِنْهُمْ ۖ قَالُوا لَا تَخَفْ ۖ خَصْمَانِ بَغَىٰ بَعْضُنَا عَلَىٰ بَعْضٍ فَاحْكُم بَيْنَنَا بِالْحَقِّ وَلَا تُشْطِطْ وَاهْدِنَا إِلَىٰ سَوَاءِ الصِّرَاطِ
Swahili
 
Walipo muingilia Daudi, naye akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Sisi ni wagombanao wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuongoe kwenye njia iliyo sawa.

Ayah  38:23  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ هَٰذَا أَخِي لَهُ تِسْعٌ وَتِسْعُونَ نَعْجَةً وَلِيَ نَعْجَةٌ وَاحِدَةٌ فَقَالَ أَكْفِلْنِيهَا وَعَزَّنِي فِي الْخِطَابِ
Swahili
 
Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo wa kike tisiini na tisa; na mimi ninaye kondoo mke mmoja. Akasema: Nipe huyo nikufugie! Na amenishinda kwa maneno.

Ayah  38:24  الأية
    +/- -/+  
قَالَ لَقَدْ ظَلَمَكَ بِسُؤَالِ نَعْجَتِكَ إِلَىٰ نِعَاجِهِ ۖ وَإِنَّ كَثِيرًا مِّنَ الْخُلَطَاءِ لَيَبْغِي بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَقَلِيلٌ مَّا هُمْ ۗ وَظَنَّ دَاوُودُ أَنَّمَا فَتَنَّاهُ فَاسْتَغْفَرَ رَبَّهُ وَخَرَّ رَاكِعًا وَأَنَابَ ۩
Swahili
 
Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake. Na hakika washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao, isipo kuwa walio amini na wakatenda mema. Na hao ni wachache. Na Daudi akajua kuwa tumemfanyia mtihani. Basi akamwomba msamaha Mola wake Mlezi, na akaanguka kusujudu na kutubia.

Ayah  38:25  الأية
    +/- -/+  
فَغَفَرْنَا لَهُ ذَٰلِكَ ۖ وَإِنَّ لَهُ عِندَنَا لَزُلْفَىٰ وَحُسْنَ مَآبٍ
Swahili
 
Basi tukamsamehe kwa hayo. Naye kwa hakika anao mkaribisho mkubwa na marejeo mazuri kwetu.

Ayah  38:26  الأية
    +/- -/+  
يَا دَاوُودُ إِنَّا جَعَلْنَاكَ خَلِيفَةً فِي الْأَرْضِ فَاحْكُم بَيْنَ النَّاسِ بِالْحَقِّ وَلَا تَتَّبِعِ الْهَوَىٰ فَيُضِلَّكَ عَن سَبِيلِ اللهِ ۚ إِنَّ الَّذِينَ يَضِلُّونَ عَن سَبِيلِ اللهِ لَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ بِمَا نَسُوا يَوْمَ الْحِسَابِ
Swahili
 
Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya wewe uwe Khalifa katika nchi. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika wanao ipotea Njia ya Mwenyezi Mungu wakaiacha, watapata adhabu kali kwa sababu ya kusahau kwao Siku ya Hisabu.

Ayah  38:27  الأية
    +/- -/+  
وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاءَ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا بَاطِلًا ۚ ذَٰلِكَ ظَنُّ الَّذِينَ كَفَرُوا ۚ فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِنَ النَّارِ
Swahili
 
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na viliomo ndani yao bure. Hiyo ni dhana ya walio kufuru. Ole wao walio kufuru kwa Moto utao wapata.

Ayah  38:28  الأية
    +/- -/+  
أَمْ نَجْعَلُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ كَالْمُفْسِدِينَ فِي الْأَرْضِ أَمْ نَجْعَلُ الْمُتَّقِينَ كَالْفُجَّارِ
Swahili
 
Je! Tuwafanye walio amini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika nchi? Au tuwafanye wachamngu kama waovu?

Ayah  38:29  الأية
    +/- -/+  
كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ مُبَارَكٌ لِّيَدَّبَّرُوا آيَاتِهِ وَلِيَتَذَكَّرَ أُولُو الْأَلْبَابِ
Swahili
 
Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili.

Ayah  38:30  الأية
    +/- -/+  
وَوَهَبْنَا لِدَاوُودَ سُلَيْمَانَ ۚ نِعْمَ الْعَبْدُ ۖ إِنَّهُ أَوَّابٌ
Swahili
 
Na Daudi tukamtunukia Suleiman. Alikuwa mja mwema. Na hakika alikuwa mwingi wa kutubia.

Ayah  38:31  الأية
    +/- -/+  
إِذْ عُرِضَ عَلَيْهِ بِالْعَشِيِّ الصَّافِنَاتُ الْجِيَادُ
Swahili
 
Alipo pelekewa jioni farasi wasimamao kidete, tayari kutoka shoti;

Ayah  38:32  الأية
    +/- -/+  
فَقَالَ إِنِّي أَحْبَبْتُ حُبَّ الْخَيْرِ عَن ذِكْرِ رَبِّي حَتَّىٰ تَوَارَتْ بِالْحِجَابِ
Swahili
 
Basi akasema: Navipenda vitu vizuri kwa kumkumbuka Mola wangu Mlezi. Kisha wakafichikana nyuma ya boma.

Ayah  38:33  الأية
    +/- -/+  
رُدُّوهَا عَلَيَّ ۖ فَطَفِقَ مَسْحًا بِالسُّوقِ وَالْأَعْنَاقِ
Swahili
 
(Akasema:) Nirudishieni! Akaanza kuwapapasa miguu na shingo.

Ayah  38:34  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ فَتَنَّا سُلَيْمَانَ وَأَلْقَيْنَا عَلَىٰ كُرْسِيِّهِ جَسَدًا ثُمَّ أَنَابَ
Swahili
 
Na tulimtia mtihanini Suleiman, na tukauweka mwili juu ya kiti chake, kisha akarejea kwa kutubu.

Ayah  38:35  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبِّ اغْفِرْ لِي وَهَبْ لِي مُلْكًا لَّا يَنبَغِي لِأَحَدٍ مِّن بَعْدِي ۖ إِنَّكَ أَنتَ الْوَهَّابُ
Swahili
 
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nisamehe na unipe ufalme usio mwelekea yeyote baada yangu. Hakika Wewe ndiye Mpaji.

Ayah  38:36  الأية
    +/- -/+  
فَسَخَّرْنَا لَهُ الرِّيحَ تَجْرِي بِأَمْرِهِ رُخَاءً حَيْثُ أَصَابَ
Swahili
 
Basi tukaufanya upepo umtumikie, ukenda kwa amri yake, popote alipo taka kufika.

Ayah  38:37  الأية
    +/- -/+  
وَالشَّيَاطِينَ كُلَّ بَنَّاءٍ وَغَوَّاصٍ
Swahili
 
Na tukayafanya mashet'ani yamtumikie, wote wajenzi na wapiga mbizi.

Ayah  38:38  الأية
    +/- -/+  
وَآخَرِينَ مُقَرَّنِينَ فِي الْأَصْفَادِ
Swahili
 
Na wengine wafungwao kwa minyororo.

Ayah  38:39  الأية
    +/- -/+  
هَٰذَا عَطَاؤُنَا فَامْنُنْ أَوْ أَمْسِكْ بِغَيْرِ حِسَابٍ
Swahili
 
Hichi ndicho kipawa chetu. Basi toa au zuia, bila ya hisabu.

Ayah  38:40  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ لَهُ عِندَنَا لَزُلْفَىٰ وَحُسْنَ مَآبٍ
Swahili
 
Na hakika yeye kwetu Sisi ana cheo cha kukaribishwa kwetu, na pahala pazuri pa kurejea.

Ayah  38:41  الأية
    +/- -/+  
وَاذْكُرْ عَبْدَنَا أَيُّوبَ إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ أَنِّي مَسَّنِيَ الشَّيْطَانُ بِنُصْبٍ وَعَذَابٍ
Swahili
 
Na mkumbuke mja wetu Ayubu alipo mwita Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika Shet'ani amenifikishia udhia na adhabu.

Ayah  38:42  الأية
    +/- -/+  
ارْكُضْ بِرِجْلِكَ ۖ هَٰذَا مُغْتَسَلٌ بَارِدٌ وَشَرَابٌ
Swahili
 
(Akaambiwa:) Piga-piga ardhi kwa mguu wako! Basi haya maji baridi ya kuogea na ya kunywa.

Ayah  38:43  الأية
    +/- -/+  
وَوَهَبْنَا لَهُ أَهْلَهُ وَمِثْلَهُم مَّعَهُمْ رَحْمَةً مِّنَّا وَذِكْرَىٰ لِأُولِي الْأَلْبَابِ
Swahili
 
Na tukampa ahali zake na wengine kama wao pamoja nao, kuwa ni rehema itokayo kwetu, na iwe kumbusho kwa watu wenye akili.

Ayah  38:44  الأية
    +/- -/+  
وَخُذْ بِيَدِكَ ضِغْثًا فَاضْرِب بِّهِ وَلَا تَحْنَثْ ۗ إِنَّا وَجَدْنَاهُ صَابِرًا ۚ نِّعْمَ الْعَبْدُ ۖ إِنَّهُ أَوَّابٌ
Swahili
 
Na shika kicha cha vijiti tu mkononi mwako, kisha ndio upigie nacho, wala usivunje kiapo. Hakika tulimkuta mwenye subira, mbora wa waja, kwa hakika alikuwa mwingi wa kutubu.

Ayah  38:45  الأية
    +/- -/+  
وَاذْكُرْ عِبَادَنَا إِبْرَاهِيمَ وَإِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ أُولِي الْأَيْدِي وَالْأَبْصَارِ
Swahili
 
Na wakumbuke waja wetu, Ibrahim na Is-haqa na Yaa'qubu walio kuwa na nguvu na busara.

Ayah  38:46  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا أَخْلَصْنَاهُم بِخَالِصَةٍ ذِكْرَى الدَّارِ
Swahili
 
Sisi tumewakhusisha wao kwa sifa ya ukumbusho wa Akhera.

Ayah  38:47  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّهُمْ عِندَنَا لَمِنَ الْمُصْطَفَيْنَ الْأَخْيَارِ
Swahili
 
Na hakika wao kwetu sisi ni wateuliwa walio bora.

Ayah  38:48  الأية
    +/- -/+  
وَاذْكُرْ إِسْمَاعِيلَ وَالْيَسَعَ وَذَا الْكِفْلِ ۖ وَكُلٌّ مِّنَ الْأَخْيَارِ
Swahili
 
Na mkumbuke Ismail na Alyasaa na Dhulkifli, na wote hao ni katika walio bora.

Ayah  38:49  الأية
    +/- -/+  
هَٰذَا ذِكْرٌ ۚ وَإِنَّ لِلْمُتَّقِينَ لَحُسْنَ مَآبٍ
Swahili
 
Huu ni ukumbusho. Na hakika wachamngu wana marudio mazuri.

Ayah  38:50  الأية
    +/- -/+  
جَنَّاتِ عَدْنٍ مُّفَتَّحَةً لَّهُمُ الْأَبْوَابُ
Swahili
 
Bustani za milele zitazo funguliwa milango yao kwa ajili yao.

Ayah  38:51  الأية
    +/- -/+  
مُتَّكِئِينَ فِيهَا يَدْعُونَ فِيهَا بِفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ وَشَرَابٍ
Swahili
 
Humo wataegemea matakia, wawe wanaagiza humo matunda mengi na vinywaji.

Ayah  38:52  الأية
    +/- -/+  
وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ أَتْرَابٌ
Swahili
 
Na pamoja nao wake zao wenye kutuliza macho, hirimu zao.

Ayah  38:53  الأية
    +/- -/+  
هَٰذَا مَا تُوعَدُونَ لِيَوْمِ الْحِسَابِ
Swahili
 
Haya ndiyo mliyo ahidiwa kwa Siku ya Hisabu.

Ayah  38:54  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ هَٰذَا لَرِزْقُنَا مَا لَهُ مِن نَّفَادٍ
Swahili
 
Hakika hii ndiyo riziki yetu isiyo malizika.

Ayah  38:55  الأية
    +/- -/+  
هَٰذَا ۚ وَإِنَّ لِلطَّاغِينَ لَشَرَّ مَآبٍ
Swahili
 
Ndio hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marudio maovu kabisa;

Ayah  38:56  الأية
    +/- -/+  
جَهَنَّمَ يَصْلَوْنَهَا فَبِئْسَ الْمِهَادُ
Swahili
 
Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia.

Ayah  38:57  الأية
    +/- -/+  
هَٰذَا فَلْيَذُوقُوهُ حَمِيمٌ وَغَسَّاقٌ
Swahili
 
Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha!

Ayah  38:58  الأية
    +/- -/+  

Ayah  38:59  الأية
    +/- -/+  
هَٰذَا فَوْجٌ مُّقْتَحِمٌ مَّعَكُمْ ۖ لَا مَرْحَبًا بِهِمْ ۚ إِنَّهُمْ صَالُو النَّارِ
Swahili
 
Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni.

Ayah  38:60  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا بَلْ أَنتُمْ لَا مَرْحَبًا بِكُمْ ۖ أَنتُمْ قَدَّمْتُمُوهُ لَنَا ۖ فَبِئْسَ الْقَرَارُ
Swahili
 
Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi ndio mlio tusabibisha haya, napo ni pahala paovu kabisa!

Ayah  38:61  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا رَبَّنَا مَن قَدَّمَ لَنَا هَٰذَا فَزِدْهُ عَذَابًا ضِعْفًا فِي النَّارِ
Swahili
 
Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusabibisha haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni.

Ayah  38:62  الأية
    +/- -/+  
وَقَالُوا مَا لَنَا لَا نَرَىٰ رِجَالًا كُنَّا نَعُدُّهُم مِّنَ الْأَشْرَارِ
Swahili
 
Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahisabu ndio katika waovu?

Ayah  38:63  الأية
    +/- -/+  
أَتَّخَذْنَاهُمْ سِخْرِيًّا أَمْ زَاغَتْ عَنْهُمُ الْأَبْصَارُ
Swahili
 
Tulikosea tulipo wafanyia maskhara, au macho yetu tu hayawaoni ?

Ayah  38:64  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ ذَٰلِكَ لَحَقٌّ تَخَاصُمُ أَهْلِ النَّارِ
Swahili
 
Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni.

Ayah  38:65  الأية
    +/- -/+  
قُلْ إِنَّمَا أَنَا مُنذِرٌ ۖ وَمَا مِنْ إِلَٰهٍ إِلَّا اللهُ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ
Swahili
 
Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenda nguvu,

Ayah  38:66  الأية
    +/- -/+  
رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الْعَزِيزُ الْغَفَّارُ
Swahili
 
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na viliomo baina yake, Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe.

Ayah  38:67  الأية
    +/- -/+  

Ayah  38:68  الأية
    +/- -/+  

Ayah  38:69  الأية
    +/- -/+  
مَا كَانَ لِيَ مِنْ عِلْمٍ بِالْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ إِذْ يَخْتَصِمُونَ
Swahili
 
Sikuwa na ilimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipo kuwa wakishindana.

Ayah  38:70  الأية
    +/- -/+  
إِن يُوحَىٰ إِلَيَّ إِلَّا أَنَّمَا أَنَا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Haikufunuliwa kwangu isipo kuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhaahiri.

Ayah  38:71  الأية
    +/- -/+  
إِذْ قَالَ رَبُّكَ لِلْمَلَائِكَةِ إِنِّي خَالِقٌ بَشَرًا مِّن طِينٍ
Swahili
 
Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo.

Ayah  38:72  الأية
    +/- -/+  
فَإِذَا سَوَّيْتُهُ وَنَفَخْتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُوا لَهُ سَاجِدِينَ
Swahili
 
Na nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa kumt'ii.

Ayah  38:73  الأية
    +/- -/+  
فَسَجَدَ الْمَلَائِكَةُ كُلُّهُمْ أَجْمَعُونَ
Swahili
 
Basi Malaika wakat'ii wote pamoja.

Ayah  38:74  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا إِبْلِيسَ اسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri.

Ayah  38:75  الأية
    +/- -/+  
قَالَ يَا إِبْلِيسُ مَا مَنَعَكَ أَن تَسْجُدَ لِمَا خَلَقْتُ بِيَدَيَّ ۖ أَسْتَكْبَرْتَ أَمْ كُنتَ مِنَ الْعَالِينَ
Swahili
 
Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumt'ii yule niliye muumba kwa mikono yangu? Je! Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?

Ayah  38:76  الأية
    +/- -/+  
قَالَ أَنَا خَيْرٌ مِّنْهُ ۖ خَلَقْتَنِي مِن نَّارٍ وَخَلَقْتَهُ مِن طِينٍ
Swahili
 
Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo.

Ayah  38:77  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فَاخْرُجْ مِنْهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٌ
Swahili
 
Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika.

Ayah  38:78  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ عَلَيْكَ لَعْنَتِي إِلَىٰ يَوْمِ الدِّينِ
Swahili
 
Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo.

Ayah  38:79  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبِّ فَأَنظِرْنِي إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ
Swahili
 
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watayo fufuliwa viumbe.

Ayah  38:80  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ الْمُنظَرِينَ
Swahili
 
Mwenyezi Mungu akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa walio pewa muhula,

Ayah  38:81  الأية
    +/- -/+  

Ayah  38:82  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فَبِعِزَّتِكَ لَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote,

Ayah  38:83  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا عِبَادَكَ مِنْهُمُ الْمُخْلَصِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio khitariwa.

Ayah  38:84  الأية
    +/- -/+  

Ayah  38:85  الأية
    +/- -/+  
لَأَمْلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكَ وَمِمَّن تَبِعَكَ مِنْهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao wote wenye kukufuata miongoni mwao.

Ayah  38:86  الأية
    +/- -/+  
قُلْ مَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُتَكَلِّفِينَ
Swahili
 
Sema (Ewe Mtume) : Sikuombeni ujira juu ya haya, wala mimi si katika wadanganyifu.

Ayah  38:87  الأية
    +/- -/+  
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ
Swahili
 
Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu wote.

Ayah  38:88  الأية
    +/- -/+  
وَلَتَعْلَمُنَّ نَبَأَهُ بَعْدَ حِينٍ
Swahili
 
Na bila ya shaka mtajua khabari zake baada ya muda.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us