Prev  

44. Surah Ad-Dukhân سورة الدّخان

  Next  





Ayah  44:3  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ
Swahili
 
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.

Ayah  44:4  الأية
    +/- -/+  
فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ
Swahili
 
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,

Ayah  44:5  الأية
    +/- -/+  
أَمْرًا مِّنْ عِندِنَا ۚ إِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ
Swahili
 
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.

Ayah  44:6  الأية
    +/- -/+  
رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ ۚ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
Swahili
 
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.

Ayah  44:7  الأية
    +/- -/+  
رَبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Swahili
 
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.

Ayah  44:8  الأية
    +/- -/+  
لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْيِي وَيُمِيتُ ۖ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.

Ayah  44:9  الأية
    +/- -/+  

Ayah  44:10  الأية
    +/- -/+  
فَارْتَقِبْ يَوْمَ تَأْتِي السَّمَاءُ بِدُخَانٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,

Ayah  44:11  الأية
    +/- -/+  
يَغْشَى النَّاسَ ۖ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٌ
Swahili
 
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!

Ayah  44:12  الأية
    +/- -/+  
رَّبَّنَا اكْشِفْ عَنَّا الْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ
Swahili
 
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.

Ayah  44:13  الأية
    +/- -/+  
أَنَّىٰ لَهُمُ الذِّكْرَىٰ وَقَدْ جَاءَهُمْ رَسُولٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.

Ayah  44:14  الأية
    +/- -/+  
ثُمَّ تَوَلَّوْا عَنْهُ وَقَالُوا مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ
Swahili
 
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.

Ayah  44:15  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا كَاشِفُو الْعَذَابِ قَلِيلًا ۚ إِنَّكُمْ عَائِدُونَ
Swahili
 
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!

Ayah  44:16  الأية
    +/- -/+  
يَوْمَ نَبْطِشُ الْبَطْشَةَ الْكُبْرَىٰ إِنَّا مُنتَقِمُونَ
Swahili
 
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.

Ayah  44:17  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ فَتَنَّا قَبْلَهُمْ قَوْمَ فِرْعَوْنَ وَجَاءَهُمْ رَسُولٌ كَرِيمٌ
Swahili
 
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.

Ayah  44:18  الأية
    +/- -/+  
أَنْ أَدُّوا إِلَيَّ عِبَادَ اللهِ ۖ إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ
Swahili
 
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.

Ayah  44:19  الأية
    +/- -/+  
وَأَن لَّا تَعْلُوا عَلَى اللهِ ۖ إِنِّي آتِيكُم بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.

Ayah  44:20  الأية
    +/- -/+  
وَإِنِّي عُذْتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمْ أَن تَرْجُمُونِ
Swahili
 
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.

Ayah  44:21  الأية
    +/- -/+  
وَإِن لَّمْ تُؤْمِنُوا لِي فَاعْتَزِلُونِ
Swahili
 
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.

Ayah  44:22  الأية
    +/- -/+  
فَدَعَا رَبَّهُ أَنَّ هَٰؤُلَاءِ قَوْمٌ مُّجْرِمُونَ
Swahili
 
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.

Ayah  44:23  الأية
    +/- -/+  
فَأَسْرِ بِعِبَادِي لَيْلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Swahili
 
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.

Ayah  44:24  الأية
    +/- -/+  
وَاتْرُكِ الْبَحْرَ رَهْوًا ۖ إِنَّهُمْ جُندٌ مُّغْرَقُونَ
Swahili
 
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.

Ayah  44:25  الأية
    +/- -/+  
كَمْ تَرَكُوا مِن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
 
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!


Ayah  44:27  الأية
    +/- -/+  
وَنَعْمَةٍ كَانُوا فِيهَا فَاكِهِينَ
Swahili
 
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!

Ayah  44:28  الأية
    +/- -/+  
كَذَٰلِكَ ۖ وَأَوْرَثْنَاهَا قَوْمًا آخَرِينَ
Swahili
 
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.

Ayah  44:29  الأية
    +/- -/+  
فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ السَّمَاءُ وَالْأَرْضُ وَمَا كَانُوا مُنظَرِينَ
Swahili
 
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.

Ayah  44:30  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدْ نَجَّيْنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ مِنَ الْعَذَابِ الْمُهِينِ
Swahili
 
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,

Ayah  44:31  الأية
    +/- -/+  
مِن فِرْعَوْنَ ۚ إِنَّهُ كَانَ عَالِيًا مِّنَ الْمُسْرِفِينَ
Swahili
 
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.

Ayah  44:32  الأية
    +/- -/+  
وَلَقَدِ اخْتَرْنَاهُمْ عَلَىٰ عِلْمٍ عَلَى الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.

Ayah  44:33  الأية
    +/- -/+  
وَآتَيْنَاهُم مِّنَ الْآيَاتِ مَا فِيهِ بَلَاءٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.


Ayah  44:35  الأية
    +/- -/+  
إِنْ هِيَ إِلَّا مَوْتَتُنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُنشَرِينَ
Swahili
 
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.

Ayah  44:36  الأية
    +/- -/+  
فَأْتُوا بِآبَائِنَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
Swahili
 
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.

Ayah  44:37  الأية
    +/- -/+  
أَهُمْ خَيْرٌ أَمْ قَوْمُ تُبَّعٍ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ أَهْلَكْنَاهُمْ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا مُجْرِمِينَ
Swahili
 
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.

Ayah  44:38  الأية
    +/- -/+  
وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَاعِبِينَ
Swahili
 
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.

Ayah  44:39  الأية
    +/- -/+  
مَا خَلَقْنَاهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ
Swahili
 
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.

Ayah  44:40  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ مِيقَاتُهُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.

Ayah  44:41  الأية
    +/- -/+  
يَوْمَ لَا يُغْنِي مَوْلًى عَن مَّوْلًى شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ
Swahili
 
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.

Ayah  44:42  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا مَن رَّحِمَ اللهُ ۚ إِنَّهُ هُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.



Ayah  44:45  الأية
    +/- -/+  
كَالْمُهْلِ يَغْلِي فِي الْبُطُونِ
Swahili
 
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni


Ayah  44:47  الأية
    +/- -/+  
خُذُوهُ فَاعْتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَاءِ الْجَحِيمِ
Swahili
 
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!

Ayah  44:48  الأية
    +/- -/+  
ثُمَّ صُبُّوا فَوْقَ رَأْسِهِ مِنْ عَذَابِ الْحَمِيمِ
Swahili
 
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.

Ayah  44:49  الأية
    +/- -/+  
ذُقْ إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْكَرِيمُ
Swahili
 
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!

Ayah  44:50  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِ تَمْتَرُونَ
Swahili
 
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.

Ayah  44:51  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٍ
Swahili
 
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,


Ayah  44:53  الأية
    +/- -/+  
يَلْبَسُونَ مِن سُندُسٍ وَإِسْتَبْرَقٍ مُّتَقَابِلِينَ
Swahili
 
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,

Ayah  44:54  الأية
    +/- -/+  
كَذَٰلِكَ وَزَوَّجْنَاهُم بِحُورٍ عِينٍ
Swahili
 
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.

Ayah  44:55  الأية
    +/- -/+  
يَدْعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَاكِهَةٍ آمِنِينَ
Swahili
 
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.

Ayah  44:56  الأية
    +/- -/+  
لَا يَذُوقُونَ فِيهَا الْمَوْتَ إِلَّا الْمَوْتَةَ الْأُولَىٰ ۖ وَوَقَاهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ
Swahili
 
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,

Ayah  44:57  الأية
    +/- -/+  
فَضْلًا مِّن رَّبِّكَ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ
Swahili
 
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

Ayah  44:58  الأية
    +/- -/+  
فَإِنَّمَا يَسَّرْنَاهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ
Swahili
 
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.

Ayah  44:59  الأية
    +/- -/+  
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us