Na wanapo kutana na walio amini husema: Tumeamini. Na wanapo kuwa peke yao na
mashet'ani wao husema: Hakika sisi tu pamoja nanyi. Hakika sisi tunawadhihaki tu.
Mfano wao ni kama mfano wa aliye koka moto, na ulipo tanda mwangaza wake kote
kote Mwenyezi Mungu aliiondoa nuru yao na akawawacha katika giza, hawaoni.
Au ni kama mvua kubwa itokayo mbinguni, ina giza na radi na umeme; wakawa
wakitia vidole vyao masikioni mwao kwa ajili ya mingurumo, kwa kuogopa kufa. Na
Mwenyezi Mungu amewazunguka makafiri.
Unakaribia umeme kunyakua macho yao. Kila ukiwatolea mwangaza huenda, na unapo
wafanyia giza husimama. Na angelitaka Mwenyezi Mungu angeliondoa kusikia kwao na
kuona kwao. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.
(Mwenyezi Mungu) ambaye amekufanyieni hii ardhi kuwa kama tandiko, na mbingu
kama paa, na akateremsha maji kutoka mbinguni, na kwayo akatoa matunda yawe
riziki zenu. Basi msimfanyizie Mwenyezi Mungu washirika, na hali nyinyi mnajua.
Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyo mteremshia mja wetu basi leteni sura moja ya
mfano wake, na muwaite mashahidi wenu badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa mnasema
kweli.
Na wabashirie walio amini na wakatenda mema kwamba watapata mabustani yapitayo
mito kati yake; kila watapo pewa matunda humo, watasema: Haya ndiyo kama tuliyo
pewa mbele. Na wataletewa matunda yaliyo fanana; na humo watakuwa na wake walio
takasika; na wao humo watadumu.
Hakika Mwenyezi Mungu haoni haya kutoa mfano hata wa mbu na ulio wa zaidi yake.
Ama wale walio amini hujua ya kwamba hiyo ni haki iliyo toka kwa Mola wao Mlezi,
lakini wale walio kufuru husema: Ni nini analo kusudia Mwenyezi Mungu kwa mfano
huu? Kwa mfano huu huwapoteza wengi na huwaongoa wengi; lakini hawapotezi ila
wale wapotovu,
Wanao vunja ahadi ya Mwenyezi Mungu baada ya kwisha ifunga, na wakayakata aliyo
amrisha Mwenyezi Mungu kuungwa, na wakafanya uharibifu katika nchi; hao ndio
wenye khasara.
Na pale Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Mimi nitamweka katika ardhi
Khalifa (mfwatizi), wakasema: Utaweka humo atakaye fanya uharibifu humo na
kumwaga damu, hali sisi tunakutakasa kwa sifa zako na tunakutaja kwa utakatifu
wako? Akasema: Hakika Mimi nayajua msiyo yajua.
Akasema: Ewe Adam! Waambie majina yake. Basi alipo waambia majina yake alisema:
Sikukwambieni kwamba Mimi ninajua siri za mbinguni na za duniani, na ninayajua
mnayo yadhihirisha na mliyo kuwa mnayaficha?
Na tulisema: Ewe Adam! Kaa wewe na mkeo katika Bustani, na kuleni humo maridhawa
popote mpendapo, lakini msiukaribie mti huu tu; mkawa katika wale walio dhulumu.
Lakini Shet'ani aliwatelezesha hao wawili na akawatoa katika waliyo kuwamo, na
tukasema: Shukeni, nanyi ni maadui nyinyi kwa nyinyi. Katika ardhi yatakuwa
makaazi yenu na starehe kwa muda.
Kisha Adam akapokea maneno kwa Mola wake Mlezi, na Mola wake Mlezi alimkubalia
toba yake; hakika Yeye ndiye Mwingi wa kukubali toba na Mwenye kurehemu.
Tukasema: Shukeni nyote; na kama ukikufikieni uwongofu utokao kwangu, basi
watakao fuata uwongofu wangu huo haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika.
Na aminini niliyo yateremsha ambayo yanasadikisha mliyo nayo, wala msiwe wa
kwanza kuyakataa. Wala msiuze Ishara zangu kwa thamani ndogo. Na niogopeni Mimi
tu.
Na vile tulipo kuokoeni kwa watu wa Firauni walio kupeni adhabu mbaya,
wakiwachinja wana wenu wa kiume na wakawawacha hai wanawake; na katika hayo
ulikuwa ni mtihani mkubwa ulio toka kwa Mola wenu Mlezi.
Na Musa alipo waambia watu wake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmezidhulumu
nafsi zenu kwa kuchukua kwenu ndama (kumuabudu). Basi tubuni kwa Muumba wenu na
ziueni nafsi zenu. Haya ni bora kwenu mbele ya Muumba wenu. Naye akapokea toba
yenu. Hakika Yeye ndiye apokeaye toba na Mwenye kurehemu.
Na tukakutilieni kivuli kwa mawingu na tukakuteremshieni Manna na Salwa;
tukakwambieni: Kuleni vitu vizuri hivi tulivyo kuruzukuni. Nao hawakutudhulumu
Sisi lakini walikuwa wanajidhulumu nafsi zao.
Na tulipo sema: Ingieni mji huu, na humo mle mpendapo maridhawa, na ingieni
katika mlango wake kwa unyenyekevu, na semeni: Tusamehe! Tutakusameheni makosa
yenu, na tutawazidishia wema wafanyao wema.
Lakini walio dhulumu waliibadili kauli isiyo kuwa waliyo ambiwa. Kwa hivyo
tukaiteremsha juu ya wale walio dhulumu adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya
walivyo kuwa wamepotoka.
Na Musa alipo omba maji kwa ajili ya watu wake, tulimwambia: Lipige jiwe kwa
fimbo yako. Mara zikatimbuka chemchem kumi na mbili; kila kabila ikajua mahali
pake pa kunywea. Tukawaambia: Kuleni na mnywe riziki ya Mwenyezi Mungu, wala
msiasi katika nchi mkafanya uharibifu.
Na mlipo sema: Ewe Musa! Hatuwezi kuvumilia chakula cha namna moja tu, basi
tuombee kwa Mola wako Mlezi atutolee vile vinavyo mea katika ardhi, kama mboga
zake, na matango yake, na thom zake, na adesi zake, na vitunguu vyake. Akasema:
Mnabadili kilicho duni kwa kilicho bora? Shukeni mjini, huko mtapata mlivyo
viomba. Na wakapigwa na unyonge,na umasikini, na wakastahili ghadhabu ya
Mwenyezi Mungu. Na haya ni kwa sababu walikuwa wakiyakataa maneno ya Mwenyezi
Mungu, na wakiwauwa Manabii pasipo haki. Hayo ni kwa walivyo asi na wakapindukia
mipaka.
Hakika Walio amini, na Mayahudi na Wakristo, na Wasabai; yeyote atakaye muamini
Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na akatenda mema basi watapata malipwa yao kwa
Mola wao Mlezi, wala haitakuwa khofu juu yao, wala hawatahuzunika.
Na tulipo chukua ahadi yenu, na tukaunyanyua mlima juu yenu (tukakwambieni):
Shikeni kwa nguvu haya tuliyo kupeni, na yakumbukeni yaliyomo ndani yake ili
mpate kujilinda.
Na Musa alipo waambia watu wake: Hakika Mwenyezi Mungu anakuamrisheni mchinje
ng'ombe. Wakasema: Je! Unatufanyia mzaha? Akasema: Audhubil lahi! Najikinga kwa
Mwenyezi Mungu nisiwe miongoni mwa wajinga.
Wakasema: Tuombee kwa Mola wako Mlezi atupambanulie ni ng'ombe gani? Akasema:
Hakika Yeye anasema kwamba ng'ombe huyo si mpevu, wala si kinda, bali ni wa
katikati baina ya hao. Basi fanyeni mnavyo amrishwa.
Wakasema: Tuombee kwa Mola wako atupambanulie nini rangi yake? Akasema: Yeye
anasema, kuwa ng'ombe huyo ni wa manjano, na rangi yake imekoza, huwapendeza
wanao mtazama.
Wakasema: Tuombee kwa Mola wako Mlezi atupambanulie ni yupi? Hakika tunaona
ng'ombe wamefanana. Na kwa yakini, Inshaallah, Mwenyezi Mungu akipenda,
tutaongoka.
Akasema: Yeye anasema: Kuwa huyo ni ng'ombe asiye tiwa kazini kulima ardhi wala
kumwagia maji mimea, mzima, hana baka. Wakasema: Sasa umeleta haki. Basi
wakamchinja, na walikaribia kuwa wasifanye hayo.
Kisha nyoyo zenu zikawa ngumu baada ya hayo, hata zikawa kama mawe au ngumu
zaidi; kwani kuna mawe yanayo timbuka mito, na kuna mengine yanayo pasuka
yakatoka maji ndani yake, na kuna mengine huanguka kwa sababu ya khofu ya
Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na mnayo yafanya.
Na wanapo kutana na wale walio amini husema: Tumeamini. Na wanapo kuwa peke yao,
wao kwa wao, husema: Mnawaambia aliyo kufunulieni Mwenyezi Mungu ili wapate
kukuhojieni mbele ya Mola wenu Mlezi? Basi hamfahamu nyinyi?
Basi ole wao wanao andika kitabu kwa mikono yao, kisha wakasema: Hiki kimetoka
kwa Mwenyezi Mungu, ili wachumie kwacho pato dogo. Basi ole wao kwa yale iliyo
andika mikono yao, na ole wao kwa yale wanayo yachuma.
Na walisema: Hautatugusa Moto ila kwa siku chache tu. Sema: Mmechukua ahadi kwa
Mwenyezi Mungu? Kweli Mwenyezi Mungu hatokwenda kinyume na ahadi yake. Au
mnamsingizia Mwenyezi Mungu mambo msiyo yajua?
Na tulipo funga agano na Wana wa Israili: Hamtamuabudu yeyote ila Mwenyezi
Mungu; na muwafanyie wema wazazi na jamaa na mayatima na masikini, na semeni na
watu kwa wema, na shikeni Sala, na toeni Zaka. Kisha mkageuka isipo kuwa
wachache tu katika nyinyi; na nyinyi mnapuuza.
Kisha nyinyi kwa nyinyi mnauwana, na mnawatoa baadhi yenu majumbani kwao,
mkisaidiana kwa dhambi na uadui. Na wakikujieni mateka mnawakomboa, na hali
kuwatoa mmekatazwa. Je! Mnaamini baadhi ya Kitabu na mnakataa baadhi yake? Basi
hana malipo mwenye kutenda hayo miongoni mwenu ila hizaya katika maisha ya
duniani, na Siku ya Kiyama watapelekwa kwenye adhabu kali kabisa. Na Mwenyezi
Mungu si mwenye kughafilika na yale mnayo yatenda.
Na hakika tulimpa Musa Kitabu na tukafuatisha baada yake Mitume wengine. Na
tukampa Isa, mwana wa Mariamu, hoja zilizo waziwazi, na tukamtia nguvu kwa Roho
Takatifu. Basi kila walipo kufikieni Mitume kwa yale ambayo hayapendwi na nafsi
zenu, mlijivuna; wengine mkawakanusha, na wengine mkawauwa.
Na kilipo wajia Kitabu kitokacho kwa Mwenyezi Mungu kinacho thibitisha waliyo
nayo - na wao walikuwa wakitafutia ushindi kuwashinda makafiri - yalipo wajia
yale waliyo kuwa wakiyajua waliyakanusha. Basi laana ya Mwenyezi Mungu juu ya
wakanushao!
Kiovu kweli walicho jiuzia nafsi zao, nacho ni kule kukataa kwao aliyo
yateremsha Mwenyezi Mungu, kwa ajili ya kuona maya kwa kuwa Mwenyezi Mungu
humteremshia fadhila yake amtakaye miongoni mwa waja wake. Basi wamejiletea
wenyewe ghadhabu juu ya ghadhabu. Na makafiri watapata mateso ya kudhalilisha.
Na wanapo ambiwa: Yaaminini aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu. Wao husema:
Tunaamini tuliyo teremshiwa sisi. Na huyakataa yasiyo kuwa hayo. Na hali ya kuwa
hii ndiyo Haki inayo thibitisha yale waliyo nayo wao. Sema: Mbona mliwauwa
Manabii wa Mwenyezi Mungu hapo zamani ikiwa kweli mlikuwa Waumini?
Na tulipo chukua ahadi yenu na tukauinua mlima juu yenu (tukakwambieni):
Kamateni kwa nguvu haya tuliyo kupeni na sikieni. Wakasema: Tumesikia na
tumekataa! Na wakanyweshwa nyoyoni mwao (imani ya) ndama kwa kufuru yao. Sema:
Ni uovu mno iliyo kuamrisheni imani yenu ikiwa ni wenye kuamini.
Na hakika utawaona ni wenye kuwashinda watu wote kwa pupa ya kuishi, na kuliko
washirikina. Kila mmoja wao anatamani lau angeli pewa umri wa miaka elfu. Wala
hayo ya kuzidishiwa umri hayamuondoshei adhabu; na Mwenyezi Mungu anayaona
wanayo yatenda.
Sema: Aliye kuwa ni adui wa Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Qur'ani
moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla
yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini.
Na alipo wajia Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu, mwenye kuthibitisha yale waliyo
nayo, kundi moja miongoni mwa wale walio pewa Kitabu lilitupa Kitabu cha
Mwenyezi Mungu hicho nyuma ya migongo yao kama kwamba hawajui.
Na wakafuata yale waliyo zua mashet'ani kuuzulia ufalme wa Su leiman. Na wala
Suleiman hakukufuru, bali mashet'ani ndio walio kufuru, wakiwafundisha watu
uchawi, na yaliyo teremshwa kwa Malaika wawili, Haaruta na Maaruta katika
Baabil. Wala hao hawakumfundisha yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani;
basi usikufuru. Wakajifunza kwa hao wawili yale ya kumfarikisha mtu na mkewe.
Wala hawawezi kumdhuru mtu ila kwa kutaka Mwenyezi Mungu. Na wanajifunza yatayo
wadhuru wala hayawanufaishi. Na hakika wanajua kwamba aliye khiari haya hatakuwa
na fungu lolote katika Akhera. Na hakika ni kiovu mno walicho jiuzia nafsi zao
laiti wangelijua.
Walio kufuru miongoni mwa watu wa Kitabu na washirikina hawapendi mteremshiwe
kheri yoyote kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Na Mwenyezi Mungu humkusudia kumpa
rehema yake ampendaye. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila kubwa.
Ishara yoyote tunayo ifuta au tunayo isahaulisha tunailetea iliyo bora kuliko
hiyo, au iliyo mfano wake. Hujui kwamba Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu?
Wengi miongoni mwa watu wa Kitabu wanatamani lau wange kurudisheni nyinyi muwe
makafiri baada ya kuamini kwenu, kwa ajili ya uhasidi uliomo ndani ya nafsi zao,
baada ya kwisha wapambanukia Haki. Basi sameheni na wachilieni mbali mpaka
Mwenyezi Mungu atapo leta amri yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila
kitu.
Sivyo hivyo! Yeyote anaye elekeza uso wake kwa Mwenyezi Mungu naye ni mtenda
mema, basi ana malipo yake kwa Mola wake Mlezi, wala haitakuwa khofu juu yao
wala hawatahuzunika.
Na Mayahudi husema: Wakristo hawana lao jambo. Na Wakristo husema: Mayahudi
hawana lao jambo. Na ilhali wote wanasoma Kitabu hicho hicho (Biblia). Na
kadhaalika walisema wale wasio jua kitu mfano wa kauli yao hii. Basi Mwenyezi
Mungu atahukumu baina yao Siku ya Kiyama katika yale waliyo kuwa
wakikhitilafiana.
Na ni nani dhaalimu mkubwa kuliko yule anaye zuia misikiti ya Mwenyezi Mungu
kutajwa ndani yake jina lake na akajitahidi kuiharibu? Watu hao haitawafalia
kuingia humo ila nao wanaogopa. Duniani watapata hizaya na Akhera watapata
adhabu kubwa.
Na walisema wale wasio jua kitu: Mbona Mwenyezi Mungu hasemi nasi au zikatufikia
Ishara. Kama hivyo walisema wale walio kuwa kabla yao mfano wa kauli yao hii.
Nyoyo zao zimefanana. Hakika Sisi tumeziweka wazi Ishara kwa watu wenye yakini.