Prev  

26. Surah Ash-Shu'arâ' سورة الشعراء

  Next  



Ayah  26:1  الأية
    +/- -/+  
بِسْم ِ اللهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Ayah  26:2  الأية
    +/- -/+  
تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْمُبِينِ
Swahili
 
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.

Ayah  26:3  الأية
    +/- -/+  
لَعَلَّكَ بَاخِعٌ نَّفْسَكَ أَلَّا يَكُونُوا مُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.

Ayah  26:4  الأية
    +/- -/+  
إِن نَّشَأْ نُنَزِّلْ عَلَيْهِم مِّنَ السَّمَاءِ آيَةً فَظَلَّتْ أَعْنَاقُهُمْ لَهَا خَاضِعِينَ
Swahili
 
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.

Ayah  26:5  الأية
    +/- -/+  
وَمَا يَأْتِيهِم مِّن ذِكْرٍ مِّنَ الرَّحْمَٰنِ مُحْدَثٍ إِلَّا كَانُوا عَنْهُ مُعْرِضِينَ
Swahili
 
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.

Ayah  26:6  الأية
    +/- -/+  
فَقَدْ كَذَّبُوا فَسَيَأْتِيهِمْ أَنبَاءُ مَا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ
Swahili
 
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.

Ayah  26:7  الأية
    +/- -/+  
أَوَلَمْ يَرَوْا إِلَى الْأَرْضِ كَمْ أَنبَتْنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوْجٍ كَرِيمٍ
Swahili
 
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?

Ayah  26:8  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

Ayah  26:9  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah  26:10  الأية
    +/- -/+  
وَإِذْ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰ أَنِ ائْتِ الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ
Swahili
 
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,

Ayah  26:11  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:12  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبِّ إِنِّي أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Swahili
 
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.

Ayah  26:13  الأية
    +/- -/+  
وَيَضِيقُ صَدْرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرْسِلْ إِلَىٰ هَارُونَ
Swahili
 
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.

Ayah  26:14  الأية
    +/- -/+  
وَلَهُمْ عَلَيَّ ذَنبٌ فَأَخَافُ أَن يَقْتُلُونِ
Swahili
 
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.

Ayah  26:15  الأية
    +/- -/+  
قَالَ كَلَّا ۖ فَاذْهَبَا بِآيَاتِنَا ۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسْتَمِعُونَ
Swahili
 
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.

Ayah  26:16  الأية
    +/- -/+  
فَأْتِيَا فِرْعَوْنَ فَقُولَا إِنَّا رَسُولُ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:17  الأية
    +/- -/+  
أَنْ أَرْسِلْ مَعَنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
 
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.

Ayah  26:18  الأية
    +/- -/+  
قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ
Swahili
 
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?

Ayah  26:19  الأية
    +/- -/+  
وَفَعَلْتَ فَعْلَتَكَ الَّتِي فَعَلْتَ وَأَنتَ مِنَ الْكَافِرِينَ
Swahili
 
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?

Ayah  26:20  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فَعَلْتُهَا إِذًا وَأَنَا مِنَ الضَّالِّينَ
Swahili
 
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.

Ayah  26:21  الأية
    +/- -/+  
فَفَرَرْتُ مِنكُمْ لَمَّا خِفْتُكُمْ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكْمًا وَجَعَلَنِي مِنَ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.

Ayah  26:22  الأية
    +/- -/+  
وَتِلْكَ نِعْمَةٌ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنْ عَبَّدتَّ بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
 
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?

Ayah  26:23  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فِرْعَوْنُ وَمَا رَبُّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?

Ayah  26:24  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Swahili
 
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.

Ayah  26:25  الأية
    +/- -/+  
قَالَ لِمَنْ حَوْلَهُ أَلَا تَسْتَمِعُونَ
Swahili
 
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?

Ayah  26:26  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.

Ayah  26:27  الأية
    +/- -/+  
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ الَّذِي أُرْسِلَ إِلَيْكُمْ لَمَجْنُونٌ
Swahili
 
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.

Ayah  26:28  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبُّ الْمَشْرِقِ وَالْمَغْرِبِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ
Swahili
 
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.

Ayah  26:29  الأية
    +/- -/+  
قَالَ لَئِنِ اتَّخَذْتَ إِلَٰهًا غَيْرِي لَأَجْعَلَنَّكَ مِنَ الْمَسْجُونِينَ
Swahili
 
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.

Ayah  26:30  الأية
    +/- -/+  
قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكَ بِشَيْءٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?

Ayah  26:31  الأية
    +/- -/+  
قَالَ فَأْتِ بِهِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Swahili
 
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.

Ayah  26:32  الأية
    +/- -/+  
فَأَلْقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعْبَانٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.

Ayah  26:33  الأية
    +/- -/+  
وَنَزَعَ يَدَهُ فَإِذَا هِيَ بَيْضَاءُ لِلنَّاظِرِينَ
Swahili
 
Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.

Ayah  26:34  الأية
    +/- -/+  
قَالَ لِلْمَلَإِ حَوْلَهُ إِنَّ هَٰذَا لَسَاحِرٌ عَلِيمٌ
Swahili
 
(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.

Ayah  26:35  الأية
    +/- -/+  
يُرِيدُ أَن يُخْرِجَكُم مِّنْ أَرْضِكُم بِسِحْرِهِ فَمَاذَا تَأْمُرُونَ
Swahili
 
Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?

Ayah  26:36  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا أَرْجِهْ وَأَخَاهُ وَابْعَثْ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ
Swahili
 
Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.

Ayah  26:37  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:38  الأية
    +/- -/+  
فَجُمِعَ السَّحَرَةُ لِمِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
Swahili
 
Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.

Ayah  26:39  الأية
    +/- -/+  
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ
Swahili
 
Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?

Ayah  26:40  الأية
    +/- -/+  
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ السَّحَرَةَ إِن كَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ
Swahili
 
Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.

Ayah  26:41  الأية
    +/- -/+  
فَلَمَّا جَاءَ السَّحَرَةُ قَالُوا لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ الْغَالِبِينَ
Swahili
 
Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?

Ayah  26:42  الأية
    +/- -/+  
قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ الْمُقَرَّبِينَ
Swahili
 
Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.

Ayah  26:43  الأية
    +/- -/+  
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰ أَلْقُوا مَا أَنتُم مُّلْقُونَ
Swahili
 
Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.

Ayah  26:44  الأية
    +/- -/+  
فَأَلْقَوْا حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ الْغَالِبُونَ
Swahili
 
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.

Ayah  26:45  الأية
    +/- -/+  
فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ
Swahili
 
Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.

Ayah  26:46  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:47  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا آمَنَّا بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:48  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:49  الأية
    +/- -/+  
قَالَ آمَنتُمْ لَهُ قَبْلَ أَنْ آذَنَ لَكُمْ ۖ إِنَّهُ لَكَبِيرُكُمُ الَّذِي عَلَّمَكُمُ السِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَافٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
(Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.

Ayah  26:50  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا لَا ضَيْرَ ۖ إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Swahili
 
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

Ayah  26:51  الأية
    +/- -/+  
إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَايَانَا أَن كُنَّا أَوَّلَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.

Ayah  26:52  الأية
    +/- -/+  
وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِي إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Swahili
 
Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.

Ayah  26:53  الأية
    +/- -/+  
فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ
Swahili
 
Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.

Ayah  26:54  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ
Swahili
 
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.

Ayah  26:55  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:56  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:57  الأية
    +/- -/+  
فَأَخْرَجْنَاهُم مِّن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
Swahili
 
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,

Ayah  26:58  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:59  الأية
    +/- -/+  
كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَاهَا بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
 
Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.

Ayah  26:60  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:61  الأية
    +/- -/+  
فَلَمَّا تَرَاءَى الْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَابُ مُوسَىٰ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ
Swahili
 
Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!

Ayah  26:62  الأية
    +/- -/+  
قَالَ كَلَّا ۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهْدِينِ
Swahili
 
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!

Ayah  26:63  الأية
    +/- -/+  
فَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنِ اضْرِب بِّعَصَاكَ الْبَحْرَ ۖ فَانفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَالطَّوْدِ الْعَظِيمِ
Swahili
 
Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.

Ayah  26:64  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:65  الأية
    +/- -/+  
وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.

Ayah  26:66  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:67  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.

Ayah  26:68  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah  26:69  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:70  الأية
    +/- -/+  
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَا تَعْبُدُونَ
Swahili
 
Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?

Ayah  26:71  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَاكِفِينَ
Swahili
 
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.

Ayah  26:72  الأية
    +/- -/+  
قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ
Swahili
 
Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?

Ayah  26:73  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:74  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا بَلْ وَجَدْنَا آبَاءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ
Swahili
 
Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.

Ayah  26:75  الأية
    +/- -/+  
قَالَ أَفَرَأَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Swahili
 
Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-

Ayah  26:76  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:77  الأية
    +/- -/+  
فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّي إِلَّا رَبَّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:78  الأية
    +/- -/+  
الَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهْدِينِ
Swahili
 
Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,

Ayah  26:79  الأية
    +/- -/+  
وَالَّذِي هُوَ يُطْعِمُنِي وَيَسْقِينِ
Swahili
 
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.

Ayah  26:80  الأية
    +/- -/+  
وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ
Swahili
 
Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.

Ayah  26:81  الأية
    +/- -/+  
وَالَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحْيِينِ
Swahili
 
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.

Ayah  26:82  الأية
    +/- -/+  
وَالَّذِي أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِي خَطِيئَتِي يَوْمَ الدِّينِ
Swahili
 
Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.

Ayah  26:83  الأية
    +/- -/+  
رَبِّ هَبْ لِي حُكْمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ
Swahili
 
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.

Ayah  26:84  الأية
    +/- -/+  
وَاجْعَل لِّي لِسَانَ صِدْقٍ فِي الْآخِرِينَ
Swahili
 
Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.

Ayah  26:85  الأية
    +/- -/+  
وَاجْعَلْنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ النَّعِيمِ
Swahili
 
Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.

Ayah  26:86  الأية
    +/- -/+  
وَاغْفِرْ لِأَبِي إِنَّهُ كَانَ مِنَ الضَّالِّينَ
Swahili
 
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.

Ayah  26:87  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:88  الأية
    +/- -/+  
يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ
Swahili
 
Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.

Ayah  26:89  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا مَنْ أَتَى اللهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ
Swahili
 
Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.

Ayah  26:90  الأية
    +/- -/+  
وَأُزْلِفَتِ الْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ
Swahili
 
Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.

Ayah  26:91  الأية
    +/- -/+  
وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ
Swahili
 
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.

Ayah  26:92  الأية
    +/- -/+  
وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ
Swahili
 
Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu

Ayah  26:93  الأية
    +/- -/+  
مِن دُونِ اللهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ
Swahili
 
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?

Ayah  26:94  الأية
    +/- -/+  
فَكُبْكِبُوا فِيهَا هُمْ وَالْغَاوُونَ
Swahili
 
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,

Ayah  26:95  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:96  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ
Swahili
 
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:

Ayah  26:97  الأية
    +/- -/+  
تَاللهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ
Swahili
 
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,

Ayah  26:98  الأية
    +/- -/+  
إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:99  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَضَلَّنَا إِلَّا الْمُجْرِمُونَ
Swahili
 
Na hawakutupoteza ila wale wakosefu.

Ayah  26:100  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:101  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:102  الأية
    +/- -/+  
فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.

Ayah  26:103  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

Ayah  26:104  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah  26:105  الأية
    +/- -/+  
كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.

Ayah  26:106  الأية
    +/- -/+  
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?

Ayah  26:107  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:108  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:109  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:110  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:111  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الْأَرْذَلُونَ
Swahili
 
Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?

Ayah  26:112  الأية
    +/- -/+  
قَالَ وَمَا عِلْمِي بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
Swahili
 
Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?

Ayah  26:113  الأية
    +/- -/+  
إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّي ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ
Swahili
 
Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!

Ayah  26:114  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:115  الأية
    +/- -/+  
إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
Swahili
 
Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.

Ayah  26:116  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ
Swahili
 
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.

Ayah  26:117  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ
Swahili
 
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.

Ayah  26:118  الأية
    +/- -/+  
فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.

Ayah  26:119  الأية
    +/- -/+  
فَأَنجَيْنَاهُ وَمَن مَّعَهُ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ
Swahili
 
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.

Ayah  26:120  الأية
    +/- -/+  
ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ الْبَاقِينَ
Swahili
 
Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.

Ayah  26:121  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.

Ayah  26:122  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah  26:123  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:124  الأية
    +/- -/+  
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?

Ayah  26:125  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:126  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:127  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:128  الأية
    +/- -/+  
أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ آيَةً تَعْبَثُونَ
Swahili
 
Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?

Ayah  26:129  الأية
    +/- -/+  
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ
Swahili
 
Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!

Ayah  26:130  الأية
    +/- -/+  
وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ
Swahili
 
Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.

Ayah  26:131  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:132  الأية
    +/- -/+  
وَاتَّقُوا الَّذِي أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ
Swahili
 
Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.

Ayah  26:133  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:134  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:135  الأية
    +/- -/+  
إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Swahili
 
Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.

Ayah  26:136  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا سَوَاءٌ عَلَيْنَا أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ الْوَاعِظِينَ
Swahili
 
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.

Ayah  26:137  الأية
    +/- -/+  
إِنْ هَٰذَا إِلَّا خُلُقُ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.

Ayah  26:138  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:139  الأية
    +/- -/+  
فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَاهُمْ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Ayah  26:140  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah  26:141  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:142  الأية
    +/- -/+  
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَالِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?

Ayah  26:143  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:144  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:145  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:146  الأية
    +/- -/+  
أَتُتْرَكُونَ فِي مَا هَاهُنَا آمِنِينَ
Swahili
 
Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?

Ayah  26:147  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:148  الأية
    +/- -/+  
وَزُرُوعٍ وَنَخْلٍ طَلْعُهَا هَضِيمٌ
Swahili
 
Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.

Ayah  26:149  الأية
    +/- -/+  
وَتَنْحِتُونَ مِنَ الْجِبَالِ بُيُوتًا فَارِهِينَ
Swahili
 
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.

Ayah  26:150  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:151  الأية
    +/- -/+  
وَلَا تُطِيعُوا أَمْرَ الْمُسْرِفِينَ
Swahili
 
Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,

Ayah  26:152  الأية
    +/- -/+  
الَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ
Swahili
 
Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.

Ayah  26:153  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ
Swahili
 
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.

Ayah  26:154  الأية
    +/- -/+  
مَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِآيَةٍ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Swahili
 
Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

Ayah  26:155  الأية
    +/- -/+  
قَالَ هَٰذِهِ نَاقَةٌ لَّهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
Swahili
 
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.

Ayah  26:156  الأية
    +/- -/+  
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Swahili
 
Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.

Ayah  26:157  الأية
    +/- -/+  
فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا نَادِمِينَ
Swahili
 
Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.

Ayah  26:158  الأية
    +/- -/+  
فَأَخَذَهُمُ الْعَذَابُ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Ayah  26:159  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah  26:160  الأية
    +/- -/+  
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.

Ayah  26:161  الأية
    +/- -/+  
إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?

Ayah  26:162  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:163  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:164  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:165  الأية
    +/- -/+  
أَتَأْتُونَ الذُّكْرَانَ مِنَ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?

Ayah  26:166  الأية
    +/- -/+  
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَاجِكُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ
Swahili
 
Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!

Ayah  26:167  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا لُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمُخْرَجِينَ
Swahili
 
Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!

Ayah  26:168  الأية
    +/- -/+  
قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ الْقَالِينَ
Swahili
 
Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.

Ayah  26:169  الأية
    +/- -/+  
رَبِّ نَجِّنِي وَأَهْلِي مِمَّا يَعْمَلُونَ
Swahili
 
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.

Ayah  26:170  الأية
    +/- -/+  
فَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ
Swahili
 
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,

Ayah  26:171  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ
Swahili
 
Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.

Ayah  26:172  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:173  الأية
    +/- -/+  
وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا ۖ فَسَاءَ مَطَرُ الْمُنذَرِينَ
Swahili
 
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.

Ayah  26:174  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Ayah  26:175  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

Ayah  26:176  الأية
    +/- -/+  
كَذَّبَ أَصْحَابُ الْأَيْكَةِ الْمُرْسَلِينَ
Swahili
 
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.

Ayah  26:177  الأية
    +/- -/+  
إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Swahili
 
Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?

Ayah  26:178  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:179  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:180  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:181  الأية
    +/- -/+  
أَوْفُوا الْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا مِنَ الْمُخْسِرِينَ
Swahili
 
Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.

Ayah  26:182  الأية
    +/- -/+  
وَزِنُوا بِالْقِسْطَاسِ الْمُسْتَقِيمِ
Swahili
 
Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;

Ayah  26:183  الأية
    +/- -/+  
وَلَا تَبْخَسُوا النَّاسَ أَشْيَاءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا فِي الْأَرْضِ مُفْسِدِينَ
Swahili
 
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.

Ayah  26:184  الأية
    +/- -/+  
وَاتَّقُوا الَّذِي خَلَقَكُمْ وَالْجِبِلَّةَ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.

Ayah  26:185  الأية
    +/- -/+  
قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ
Swahili
 
Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.

Ayah  26:186  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ الْكَاذِبِينَ
Swahili
 
Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.

Ayah  26:187  الأية
    +/- -/+  
فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًا مِّنَ السَّمَاءِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ
Swahili
 
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

Ayah  26:188  الأية
    +/- -/+  
قَالَ رَبِّي أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ
Swahili
 
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.

Ayah  26:189  الأية
    +/- -/+  
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ الظُّلَّةِ ۚ إِنَّهُ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ
Swahili
 
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.

Ayah  26:190  الأية
    +/- -/+  
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ
Swahili
 
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

Ayah  26:191  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ
Swahili
 
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah  26:192  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّهُ لَتَنزِيلُ رَبِّ الْعَالَمِينَ
Swahili
 
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

Ayah  26:193  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:194  الأية
    +/- -/+  
عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ الْمُنذِرِينَ
Swahili
 
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,

Ayah  26:195  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:196  الأية
    +/- -/+  
وَإِنَّهُ لَفِي زُبُرِ الْأَوَّلِينَ
Swahili
 
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.

Ayah  26:197  الأية
    +/- -/+  
أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ آيَةً أَن يَعْلَمَهُ عُلَمَاءُ بَنِي إِسْرَائِيلَ
Swahili
 
Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?

Ayah  26:198  الأية
    +/- -/+  
وَلَوْ نَزَّلْنَاهُ عَلَىٰ بَعْضِ الْأَعْجَمِينَ
Swahili
 
Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,

Ayah  26:199  الأية
    +/- -/+  
فَقَرَأَهُ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا بِهِ مُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.

Ayah  26:200  الأية
    +/- -/+  
كَذَٰلِكَ سَلَكْنَاهُ فِي قُلُوبِ الْمُجْرِمِينَ
Swahili
 
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.

Ayah  26:201  الأية
    +/- -/+  
لَا يُؤْمِنُونَ بِهِ حَتَّىٰ يَرَوُا الْعَذَابَ الْأَلِيمَ
Swahili
 
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.

Ayah  26:202  الأية
    +/- -/+  
فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ
Swahili
 
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.

Ayah  26:203  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:204  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:205  الأية
    +/- -/+  
أَفَرَأَيْتَ إِن مَّتَّعْنَاهُمْ سِنِينَ
Swahili
 
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,

Ayah  26:206  الأية
    +/- -/+  
ثُمَّ جَاءَهُم مَّا كَانُوا يُوعَدُونَ
Swahili
 
Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,

Ayah  26:207  الأية
    +/- -/+  
مَا أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا يُمَتَّعُونَ
Swahili
 
Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?

Ayah  26:208  الأية
    +/- -/+  
وَمَا أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
Swahili
 
Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji -

Ayah  26:209  الأية
    +/- -/+  
ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَالِمِينَ
Swahili
 
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.

Ayah  26:210  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:211  الأية
    +/- -/+  
وَمَا يَنبَغِي لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ
Swahili
 
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.

Ayah  26:212  الأية
    +/- -/+  
إِنَّهُمْ عَنِ السَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ
Swahili
 
Hakika hao wametengwa na kusikia.

Ayah  26:213  الأية
    +/- -/+  
فَلَا تَدْعُ مَعَ اللهِ إِلَٰهًا آخَرَ فَتَكُونَ مِنَ الْمُعَذَّبِينَ
Swahili
 
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.

Ayah  26:214  الأية
    +/- -/+  
وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ
Swahili
 
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.

Ayah  26:215  الأية
    +/- -/+  
وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
Swahili
 
Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.

Ayah  26:216  الأية
    +/- -/+  
فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّي بَرِيءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ
Swahili
 
Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.

Ayah  26:217  الأية
    +/- -/+  
وَتَوَكَّلْ عَلَى الْعَزِيزِ الرَّحِيمِ
Swahili
 
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

Ayah  26:218  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:219  الأية
    +/- -/+  

Ayah  26:220  الأية
    +/- -/+  
إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
Swahili
 
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.

Ayah  26:221  الأية
    +/- -/+  
هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ الشَّيَاطِينُ
Swahili
 
Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?

Ayah  26:222  الأية
    +/- -/+  
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ
Swahili
 
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.

Ayah  26:223  الأية
    +/- -/+  
يُلْقُونَ السَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَاذِبُونَ
Swahili
 
Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.

Ayah  26:224  الأية
    +/- -/+  
وَالشُّعَرَاءُ يَتَّبِعُهُمُ الْغَاوُونَ
Swahili
 
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.

Ayah  26:225  الأية
    +/- -/+  
أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِي كُلِّ وَادٍ يَهِيمُونَ
Swahili
 
Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?

Ayah  26:226  الأية
    +/- -/+  
وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ
Swahili
 
Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?

Ayah  26:227  الأية
    +/- -/+  
إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَذَكَرُوا اللهَ كَثِيرًا وَانتَصَرُوا مِن بَعْدِ مَا ظُلِمُوا ۗ وَسَيَعْلَمُ الَّذِينَ ظَلَمُوا أَيَّ مُنقَلَبٍ يَنقَلِبُونَ
Swahili
 
Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.
 


© EsinIslam.Com Designed & produced by The Awqaf London. Please pray for us